Na MARGARET MAINA
Muda wa kuandaa: Dakika15
Muda wa mapishi: Saa 1
Walaji: 3
Vinavyohitajika
Maelekezo
Menya vitunguu maji na kata kufuatisha uviringo wake ili upate umbo la mduara kisha weka kwenye chombo.
Osha nyanya na kata vipande vinne kwa kila nyanya.
Osha karoti na kisha kwangua kiasi.
Osha na kisha kwangua kiasi cha karoti na nyingine kata vipande vidogo.
Osha koliflawa na itoe kwenye shina ili upate maua yake.
Osha majani ya giligiliani halafu uyakate.
Osha na weka njegere kwenye chombo chenye maji.
Menya tangawizi na kisha ikwangue.
Menya vitunguu saumu kisha uvitwange.
Andaa viungo vyote vya pilau pembeni tayari kutumika.
Osha na kisha andaa karafuu na pilipili.
Injika sufuria kwenye meko. Mimina mafuta ya kupikia. Weka viungo vya pilau vya unga kisha weka bizari na kaanga kwa muda kiasi.
Weka kitunguu saumu na ukoroge kiasi. Weka tangawizi na endelea kukoroga.
Weka kitunguu maji kisha koroga kwa muda kiasi. Acha viive hadi vianze kubadilika rangi.
Weka nyanya, chumvi, na pilipili manga. Koroga na kisha acha vichemke kwa dakika chache.
Weka karafuu, karoti, pilipili mboga, koliflawa na njegere. Endelea kukaanga kwa muda wa dakika kama 10 hivi.
Weka mchele huku ukiendelea kukaanga ili mchele wako uchanganyike vizuri na viungo kwenye sufuria ukiiva.
Weka maji kulingana na kiasi cha mchele wako unaoanza kuiva.
Weka moto wa wastani na kisha funika sufuria chakula kiive. Baada ya robo saa, geuza pilau kisha weka majani ya giligiliani ili kuongeza ladha na harufu nzuri ya chakula. Funika chakula ili kiendelee kuiva.
Subiri kwa muda wa dakika 10 na chakula kitakua tayari kuliwa.
Pakua na ufurahie.