Na MARGARET MAINA
Muda wa kuandaa: Dakika 15
Muda wa mapishi: Dakika 30
Walaji: 4
Vinavyohitajika
Maelekezo
Chukua wali – mchele ambao umeshaupika – uchambue vizuri kisha utie katika sahani au sinia pana. Acha upoe kabisa.
Vunja mayai matatu katika bakuli moja, kisha vunja mayai mengine mawili pamoja na maji vijiko viwili vya chakula, tia manjano kisha ziweke pembeni bakuli zako zote mbili.
Baada ya hapo, weka kikaangio au sufuria yako mekoni. Weka moto wa kiasi kisha tia mafuta ya kupikia kiasi ya vijiko viwili vya chakula. Yakipata moto, weka mayai matatu uliyoyavunja, bila viungo. Yavurugevuruge. Epua weka pembeni.
Weka tena chombo mekoni katika moto mkali, tia mafuta kijiko kimoja cha chakula. Yakipata moto, weka vitunguu na pilipili mboga kisha kaanga kwa dakika mbili.
Tia wali wako kisha geuzageuza vizuri ili wali upate moto vizuri.
Mimina mayai mabichi uliyoyakoroga na viungo juu ya wali wako kisha kaanga kwa dakika moja hadi mayai yaenee vizuri katika wali.
Chukua njegere, weka kisha koroga bila kuachia kwa muda wa dakika moja, nyunyuzia chumvi, (na sukari ukipenda) na pilipili juu ya wali wako kisha koroga vizuri kuchanganya.
Ukiona wali ni mkavu sana, mimina maji ya uvuguvugu kidogo au supu.
Baada ya hapo, acha uive vizuri kisha weka mezani tayari kuliwa.