• Nairobi
  • Last Updated May 19th, 2024 9:01 PM
Kajala atishia kuroga mchumba wa bintiye endapo atamuanika mitandaoni

Kajala atishia kuroga mchumba wa bintiye endapo atamuanika mitandaoni

NA JOHN KIMWERE

MWIGIZAJI wa Filamu za Bongo, Fridah Kajala Masanja ametishia kulaani mwanamuziki, Omary Mwanga almaarufu Marioo endapo itatokea akosane na kuachana na bintiye, Paula kisha aishie kumwanika. 

Kajala ameonya msanii huyo kuwa wakioana na pengine waachane, kamwe asianze kumuaibisha bintiye jinsi Harmonize amekuwa akiwachamba yeye na Paula kwenye mitandao.

Kajala mwenye umri wa miaka 40 ni kama amevuka mipaka zaidi kwani amemtishia Marioo kuwa iwapo atafanya hivyo, basi hatakuwa na budi ila kumroga.

Kajala aliandika hayo kwenye mtandao wake wa Instagram, huku akithibitisha kuwa mapema wiki iliyopita alipokea barua ya posa kutoka kwa Marioo akiomba idhini ya kumchumbia Paula.

Paula alitangaza kuanza mahusiano ya kimapenzi na Marioo mwezi Aprili 2023 baada ya aliyekuwa mpenziwe, Rayvanny kurudiana na mkewe Fahyma.

Kajala ameonekana waziwazi kukumbatia mahusiano ya bintiye na Marioo na hata mara nyingi ameonekana akiyapigia debe.

Hata hivyo, Kajala ameweka wazi kuwa bintiye ni mvivu na wala haelewi ikiwa atawezana na masuala ya ndoa (familia) hasa mahali palipo na wakwe zake.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, alichapisha kuwa ni balaa kwa mwanamke kuwa mvivu kisha kuishia kuolewa katika familia ina wakwe maana wanapenda kutumana tumana.

”Mwanangu ulivyo mvivu na wakwe wanavyopenda kutuma tumana utavumilia kweli?” Kajala aliandika kwenye ukurasa wake.

Kajala ambaye ni mpenzi wa zamani wa msanii Harmonize alisema kuwa anahurumia Paula, akidokeza kwamba itahitaji Mungu amsaidie kwa hilo.

La ajabu, naye Paula amepakia chapisho la mamake kwenye akaunti yake ya Instagram na kucheka tu.

 

  • Tags

You can share this post!

TikTok ipigwe marufuku Kenya – Bob Ndolo

Wakazi wa Nairobi waponea kunyofua mutura, supu na nyama ya...

T L