• Nairobi
  • Last Updated May 2nd, 2024 8:55 PM
Karen Nyamu: Nilisaidia mke wa Samidoh kupata tenda 

Karen Nyamu: Nilisaidia mke wa Samidoh kupata tenda 

NA SAMMY WAWERU 

KAREN Nyamu, ambaye ni seneta maalum amedai alisaidia aliyekuwa mke wa mwanamuziki Samuel Muchoki – Samidoh, Edday Nderitu kupata zabuni. 

Akizungumza kupitia video aliyopeperusha mbashara mitandaoni, mwanasiasa huyo wa chama cha UDA alilalamikia kuitwa ‘mvunja ndoa au kiruja njia’ akisema lawama hizo si haki kwa mtu aliyesaidia.

Matamshi yake yalionekana kutia muhuri tetesi kuwa aliwahi kusaidia Edday kujiendeleza kimaisha.

Amekuwa kwenye uhusiano haramu na Samidoh, jambo ambalo lilichangia Edday kuondoka kwenye ndoa yake ya miaka 15.

“Mimi nisaidie mtu kupata tenda kisha nilaumiwe nilivunja ndoa yake…Unadhani ninaweza kutaka asiende mbali (akimaanisha kujikuza kimaisha)?” Karen akashangaa, akijibu maswali ya wafuasi wake waliomlemea kwa madai ya kuchochea ndoa ya Samidoh kusambaratika.

Samidoh amezalisha Karen watoto wawili, na Edday watatu.

Akisisitiza kuwa ‘msaidizi’ wa Edday, mwanasiasa huyo alilalamikia wakosoaji wake kuzidi kumnyooshea kidole cha lawama kwa mikosi inayozingira familia ya Samidoh.

Mwimbaji huyo wa Mugithi, alitemwa na mkewe, Edday Nderitu ambaye Mei 2023 alisafiri Amerika.

Tayari amepata makao humo, kwa Bernice Saroni, wanawe wakianza kukata kiu cha masomo nchini humo.

Bernice ni bintiamu (cousin) wa Samidoh, na amekuwa katika mstari wa mbele kutetea Edday.

“Ninashangaa kwa nini watu wanaendelea kuniita ‘mvunja ndoa’? Mimi ni mume nilipata,” alisema.

“Ndoa yangu ndiyo inaongelelewa sana Kenya,” Karen alidai.

Alihoji amekuwa akiomba Mungu Samidoh na Edday warudiane.

 

 

  • Tags

You can share this post!

Nyani wasumbufu wanaovamia kuku na kutwanga walevi barabara...

Shamba la kuvuna upepo Marsabit

T L