• Nairobi
  • Last Updated May 2nd, 2024 8:55 PM
Karen Nyamu: Samidoh alinichagua kwa sababu huvalia maridadi 

Karen Nyamu: Samidoh alinichagua kwa sababu huvalia maridadi 

NA SAMMY WAWERU 

KAREN NYAMU mpango wa kando wa msanii wa Mugithi, Samuel Muchoki almaarufu Samidoh, ameelezea mojawapo ya sababu zilizochangia mwimbaji huyo kumchagua. 

Amesema, yeye (Karen) huvalia maridadi, hivyo basi Samidoh alivutiwa na urembo wake.

“Mimi ni mama mzuri huvalia vizuri nione kama nitaolewa,” Karen alisema.

Akitangamana na mashabiki wake mitandaoni, alionekana kupandwa na mori hasa kwa waliomkosoa kufuatia mahusiano yake haramu na Samidoh.

Baadhi wakimtaja kama mama mwenye tabia mbaya, aliwajibu akisema “nyinyi ndio mmepotoka na siku ya kiama mtanipata mbinguni nimewatangulia”.

Alisema haoni wakiurithi ufalme wa Mungu kwa sababu ya matendo yao ‘kusulubisha’ wengine.

“Nyinyi mna tabia ndio mnateseka, mnatukana wengine na mmejaa makasiriko. Mbinguni mtatupata tumewatangulia mbele yenu. Mnajifanya watakatifu na sioni hata mkiingia mbinguni,” alielezea.

Mwanasiasa huyo wa chama cha Rais William Ruto, UDA, amekuwa akilaumiwa kwa kuvunja ndoa ya Samidoh na Edday.

Wamejaaliwa kupata watoto wawili.

Samidoh amemzalisha Edday watoto watatu, na walisafiri Amerika ambako kwa sasa wanaishi.

Aidha, Samidoh amenukuliwa akibembeleza mkewe arudi.

Edday, hata hivyo, ameweka wazi kumtema msanii huyo akisisitiza kwamba hayupo tayari kuwa kwenye ndoa yenye zaidi ya mke mmoja.

 

 

 

  • Tags

You can share this post!

Vipusa 3 wakamatwa Murang’a wakinengulia walevi viuno...

Murang’a Seal juu ya jedwali huku Gor ikifinya Ulinzi

T L