• Nairobi
  • Last Updated May 4th, 2024 10:15 PM
KASHESHE: Kimenuka Wasafi

KASHESHE: Kimenuka Wasafi

NA SINDA MATIKO

KUNA demu aitwaye Aaliyah ambaye kwa kipindi kirefu amedaiwa kuwa side-chic wa Diamond Platnumz.

Sasa baada ya stori za kuwa yupo kwenye penzi zito na Zuchu, kumeripotiwa bifu kali kati ya wawili hao.

Aaliyah anadaiwa kuridhika kuwa side-chic tangu zamani kwani hata kipindi nyota huyo akiwa anamdeti Tanasha Donna, bado mrembo huyo alikuwa akimwibia.

Ila stori za kuwa Diamond anataka kumwoa Zuchu ndizo zimemuumiza. Taarifa hizi karushiwa juzi Zuchu ambaye alikuwa mwepesi wa kukana.

“Sina tatizo kabisa na Aaliyah na sijui ni kwa nini watu wanatuhusisha na ugomvi. Kiukweli Aaliyah hajawahi kunikosea chochote. Hana ubaya wowote na mimi,” Zuchu kamkingia kwenye mahojiano yake na MashamMasham.

Aidha Zuchu kwa mara nyingine kakana kuwa mpenzi wa Diamond, akisisitiza kuwa yule ni bosi wake na itabakia kuwa hivyo.

You can share this post!

KIKOLEZO: Ndoa za celebs bila jasho!

Wavinya Ndeti ajiuzulu kazi serikalini kuwinda kiti cha...

T L