• Nairobi
  • Last Updated May 9th, 2024 6:40 PM
KAULI YA WALLAH BIN WALLAH: Ukijiamini na uzingatie shughuli unayofanya bila shaka utafanikiwa sana

KAULI YA WALLAH BIN WALLAH: Ukijiamini na uzingatie shughuli unayofanya bila shaka utafanikiwa sana

NA WALLAH BIN WALLAH

WATU wengi hushindwa kufanikiwa kupata wanachohitaji maishani kwa sababu hawajiamini wala hawazingatii shughuli wanazofanya!

Wewe unafanya shughuli gani ili ufanikiwe? Kwanza kabisa unapokuwa mahali popote lazima ujiulize upo hapo ukifanya nini?

Hiyo shughuli unayoifanya hapo ina umuhimu gani kwako? Itakuongezea manufaa gani katika maisha yako? Kama unaamini ni shughuli itakayokufaidi maishani, unaifanya vizuri kweli?

Amini na kujiamini kwamba kila mtu amezaliwa kwa malengo maalum! Na kila kitu Mwenyezi Mungu amekiweka duniani kwa matumizi na madhumuni maalumu ili kishughulikiwe na kitekelezwe kwa nia na sababu maalum kwa manufaa ya maisha ya mwanadamu!

Kutambua umuhimu wa kujiamini na mazingatio ya utendakazi bila uzembe ni heshima kubwa kwa mwanadamu! Si heshima tu bali pia ni manufaa makubwa zaidi katika kuimarisha na kuboresha maisha ya kila siku ya mwanadamu!

Tumia muda wako kuelewa kwa nini upo hapo na unapaswa kufanya shughuli gani hapo ulipo! Chochote unachofanya katika maisha yako jitahidi ukifanye vizuri zaidi!

Hakuna kazi mbaya inayoleta faida duniani! Kujiamini na kujituma kufanya kazi vizuri ndiyo siri kubwa ya ufanisi maishani! Zingatia ubora wa kazi zako wakati wowote popote ulipo hata kama ni michezoni au ofisini ama shambani au darasani unapokaa ukisoma ama ukifanya mtihani wako!

Tekeleza wajibu kwa kujiamini kwamba wewe ni wewe na una uwezo wa kufanikiwa vizuri zaidi maishani!

You can share this post!

Wanyama mawindoni Klabu Bingwa CONCACAF

Sekta kuu ya bodaboda ilivyotekwa na wahalifu

T L