Na MARGARET MAINA
Muda wa kuandaa :Dakika 10
Muda wa Mapishi: Dakika 30
Walaji: 4
Unahitaji
Maelekezo
Katakata maini yawe vipande vidogo na kisha vioshe vipande hivyo halafu chuja maji na uweke kwenye sufuria.
Weka sufuria mekoni na uashe moto. Ongeza chumvi na mchanganyiko wa kitunguu saumu na tangawizi iliyosagwa.
Acha maini yachemke, ongeza maji moto pale yanapokaukia mpaka yaive kabisa.
Epua maini yako tayari kwa kuyaunga.
Chukua sufuria safi, weka kwenye moto, ongeza mafuta ya kupikia na acha yachemke kiasi kisha ongeza chumvi.
Ongeza vitunguu maji na vipike mpaka vibadilike rangi kisha ongeza mchanganyiko wa vitunguu saumu na tangawizi iliyosagwa.
Ongeza pilipili mboga na biringanya na koroga taratibu na viache viive.
Chukua karoti iliyokatwakatwa na viazi mviringo ambavyo utakuwa umevichemsha kidogo viongezee kwenye sufuria yako.
Ongeza maini yaliyochemka, pamoja na viungo unavyopendelea.
Ongeza nyanya na uache iive ili kutengeneza rojo.
Ongeza tui la nazi na koroga bila kuacha mpaka utakapoona linataka kuchemka, ila hakikisha tui halikatiki kwa kuchemka.
Epua maini yako tayari kwa kuliwa.