NA MARGARET MAINA
Muda wa kuandaa: Dakika 10
Muda wa mapishi: Dakika 40
Walaji: 4
Vinavyohitajika
Maelekezo
Ili kupika nyama ya ng’ombe na brokoli, pasha mafuta ya mizeituni kwenye sufuria juu ya moto wa kati.
Ongeza nyama iliyokatwa nyembamba na upike hadi iwe rangi ya hudhurungi, kama dakika 10.
Mara tu inapokuwa ya hudhurungi, toa kutoka kwenye sufuria na kuiweka kando.
Katika sufuria iyo hiyo, ongeza vitunguu maji vilivyokatakatwa, vitunguu saumu na vitunguu vya kijani. Pika kwa dakika moja, huku ukichochea mara kwa mara.
Kisha, ongeza brokoli na upike kwa muda wa dakika tano hadi brokoli liwe laini zaidi.
Ili kutenegeneza mchuzi, katika bakuli changanya sosi ya soya, sukari, tangawizi iliyosagwa, na pilipili.
Ongeza wanga na maji na koroga hadi vichanganyike vizuri.
Ongeza mchuzi huu kwenye sufuria na upike hadi uanze kuwa mzito, kama dakika tano hivi. Rudisha nyama ya ng’ombe na koroga ili kuchanganya, halafu pika kwa dakika mbili au tatu za ziada. Kisha, weka kando ipoe kidogo kisha pakua na ufurahie.