• Nairobi
  • Last Updated May 20th, 2024 9:16 PM
Rapudo amnunulia mkewe Amber Ray ‘nywele’ za Sh420, 000

Rapudo amnunulia mkewe Amber Ray ‘nywele’ za Sh420, 000

NA MERCY KOSKEI

MFANYABIASHARA Kennedy Rapudo ameendelea kummiminia mkewe Amber Ray zawadi za bei ghali.

Wanandoa hao walichapisha video mitandaoni wakiwa kwenye duka la wigi, na Rapudo hakusita kuchimba mfukoni mwake ili kununua wigi moja ya kifahari kwa ajili ya mpenzi wake.

Katika video hiyo, keshia wa duka hilo alionekana akionyesha kikokotoo (calculator) kinachoonyesha bei ya wigi hiyo kuwa Sh420,000.

Rapudo alionekana akitoa bunda la noti kwenye mkoba wake na kujaza nyingine kwa kadi ya ATM.

Amber Ray aliyejawa na furaha aliskika akisema kuwa anashukuru milele kwa upendo wa mumewe, huku akisema kuwa hatawahi kuchumbiana na mwanamume asiye na pesa.

“Rudia baada yangu, siwezi kamwe kuchumbiana na mwanaume asiye na hela,” aliskika akidai.

Rapudo amekuwa dhabiti katika kumpa Amber Ray maisha ya kifahari tangu kuunganishwa kwao na kuzaliwa kwa binti yao Africanah.

Mnamo Mei 2023, Rapudo aliandaa karamu ya kuwakaribisha nyumbani Amber na mtoto wao Africanah baada ya kuondoka hospitalini.

Amber alimshukuru Rapudo kwa upendo na kukiri kwamba pesa ziliwezesha hayo yote, Rapudo pia akiahidi kumnunulia Amber Ray gari jipya kabisa aina ya Range Rover.

  • Tags

You can share this post!

Msako wa walioua kinyama Kaniss na Omodollar na kuweka...

Kijana wa miaka 18 alivyomuua babake kufuatia mzozano wa...

T L