• Nairobi
  • Last Updated May 12th, 2024 5:17 PM
Riyama alichochea kipawa changu cha uigizaji-Baby D

Riyama alichochea kipawa changu cha uigizaji-Baby D

Na JOHN KIMWERE

NI miaka saba tangia aanze kujituma kwenye masuala ya uigizaji kwenye juhudi za kusaka riziki ambapo hana la ziada amepania kutinga upeo wa juu.

Anaamini anatosha mboga ambapo ameibuka kati ya wana dada wanaoendelea kuchota idadi ya wafuasi wa masuala ya filamu za waigizaji wa humu nchini. Carolyne Mwangi maarufu Baby D ni kati ya waigizaji ambao sura zao sio geni kwenye kipindi cha ‘Hulabaloo Estate.’

Kando na uigizaji ni mpishi hodari pia anamiliki duka linalopatikana jijini Nairobi la kuuza vifaa vya eletroniki ikiwamo runinga, simu za rununu na friji kati ya zinginezo. ”Ingawa nilianza kujituma kwenye masuala ya uigizaji nikiwa shuleni, tangia utotoni mwake nilidhamiria kuwa mwigizaji ambapo Riyama Selemani mzawa wa Tanzania alinichochea pakubwa na kujiunga na uigizaji,” alisema na kuongeza kuwa nusuru ahitimu kuwa mwana habari.

Pia akiwa mdogo alipenda sana kutazama kipindi cha ‘Tausi’ kilichokuwa kinapeperushwa kupitia runinga ya KBC. Katika utangulizi wake mwaka 2016 alishiriki kipindi cha ‘Jameni’ (KTN), kisha ‘Bebabeba’ (NTV) kabla ya kutua Maisha Magic ambapo hushiriki kipindi cha ‘Hulabaloo Estate.’

Anadokeza kuwa Wakenya wanazidi kupiga hatua katika uigizaji ambapo akilinganisha kazi yao na wenzie katika mataifa yanayoendelea anaweza kuipatia alama sita kwa kumi. ”Taifa hili limefurika waigizaji wengi tu wanaume na wanawake ambapo endapo wamiliki wa vyombo vya habari watashirikiana na kampuni za kusambaza filamu hakika ni hatua ikatayosaidia kutangaza kazi zetu katika mataifa mengine,” alisema.

Carolyne Mwangi maarufu Baby D…Picha/ JOHN KIMWERE

Katika mpango kutwa amepania kuanzisha brandi ya kuzalisha filamu pia kampuni ya kuzipeperusha lengo kuu likiwa kusaidia wasanii wa humu nchini wanaokuja. Anashikilia kuwa chini ya muda mrefu atakuwa anamiliki brandi iitwayo Baby D Production.

Katika tasnia ya uigizaji hakuna asiyependa kupiga shughuli na waliowatangulia. Anasema angependa kufanya kazi na mchekeshaji mahiri nchini Jackie Nyaminde maarufu Wilbroda. Afrika angependa kujipata jukwaa moja na Omotola Jalade Ekeide pia Elizabeth ‘Liz’ Benson waigizaji wa filamu za Kinigeria maarufu Nollywood. Wawili hao wanajivunia kushiriki nyingi ikiwamo ‘Blood Sisters’ ‘Alter Ego,’ na ‘Still failing,’ ‘Lizard’ mtawalia.

PANDASHUKA

Baby D anasema waigizaji hupitia changamoto kibao ikiwamo kucheleweshwa kwa mshahara, kazi zao kutopata nafasi kwenye runinga za humu nchini. Pia miaka ya sasa sekta ya uigizaji ina wasanii wengi Bali nafasi ni haba. ”Kadhalika baadhi ya stesheni za runinga nchini hupenda kutushusha maana hupenda kulipa hela zilizo chini ya bajeti ya filamu zetu,” akasema.

MAWAIDHA

Dada huyu sio mchoyo wa mawaidha, anashauri wenzie wasiwe na pupa bali wafahamu subra huvuta heri bila kuweka katika kaburi la sahau kujituma na mengine kumwachia Mola. Hata hivyo anawahimiza wawe wabunifu kama wenzao katika mataifa yanayoendelea. Katika dunia ya sasa mapenzi yamechangia kina dada wengi kutoa machozi lakini anasema kamwe hatamani kulia kwa sababu ya penzi na kudokeza kuwa hana mpenzi bali ameolewa na kazi ya usanii.

Carolyne Mwangi maarufu Baby D…JOHN KIMWERE

You can share this post!

Ulinzi Starlets yaipiga Vihiga Queens breki

Sitaki kingine ila mchujo, Shahbal akaa ngumu ODM

T L