• Nairobi
  • Last Updated April 28th, 2024 10:48 AM
Ulinzi Starlets yaipiga Vihiga Queens breki

Ulinzi Starlets yaipiga Vihiga Queens breki

Na JOHN KIMWERE

ULINZI Starlets imetoka nguvu sawa bao 1-1 dhidi ya Vihiga Queens na kuibuka timu ya pili kuvuna alama moja mbele ya wapinzani wao kwenye mechi za Ligi Kuu ya Soka la Wanawake (KWPL) muhula huu.

Gaspo Women iliyokuwa timu ya kwanza kusajili alama moja dhidi ya Vihiga Queens kwenye mechi za mkumbo wa kwanza. Vihiga ilitangulia kufunga bao hilo kupitia Phelistus Kadari kabla Ulinzi kusawazisha kupitia Siliya Rasoa. ”Nashukuru wasichana wangu kwa kujitahidi na kuzoa alama moja dhidi ya wapinzani wetu tena wakiwa kwao,” kocha wa Ulinzi Starlets, Joseph Mwanza alisema.

Naye kocha wa Vihiga alisema ”Wapinzani wetu walikuwa wamejipanga nusura watuumize.” Nao Elizabeth wambui na Iddah Adhiambo kila mmoja alitikisa wavu mara mbili na kubeba Gaspo Women kuzaba Kayole Stalerts mabao 4-1. Thika Queens ilinyuka Bunyore Starlets mabao 3-0 kupitia Lovenita Lupemba, Stella Adhiambo na Wendy Achieng.

Nao wasomi wa Sparks ya Zetech University walisajili mabao 3-1 dhidi ya Kisumu All Starlets huku Wadadia iliagana bao 1-1 na Nakuru City Queens. Licha ya matokeo hayo Vihiga ya kocha, Boniface Nyamunyamu inaongoza kwa alama 35 kutokana na mechi 13. Nayo Gaspo ilirejea katika nafasi ya pili kwa kuandikisha alama 28, mbili mbele ya Thika Queens sawa na Ulinzi Starlets tofauti ikiwa idadi ya mabao baada ya kila moja kupiga mechi 13.

You can share this post!

Wafanyakazi wa kampuni ya KPLC washtakiwa kwa wizi

Riyama alichochea kipawa changu cha uigizaji-Baby D

T L