• Nairobi
  • Last Updated May 17th, 2024 7:50 AM
Stivo Simple Boy ajinyakulia kipusa kitu kipya, Wanja Kihii

Stivo Simple Boy ajinyakulia kipusa kitu kipya, Wanja Kihii

NA RICHARD MAOSI

BAADA ya kukataliwa na rapa Kaveve Kazoze, msanii Stivo Simple Boy kwa mara nyingine amechangamsha mtandao, kwa kujinyakulia kitu kipya – Wanja Kihii.

Hii ni baada ya Wanja kuweka wazi kupitia video aliyopakia mtandaoni na kusikika akisema alikuwa tayari kufunga ndoa na Simple Boy.

“Simple Boy, mimi nakulov wewe kuja kwangu achana na hao wengine wenye unawaambia unawapenda na hawakupendi so kuja mimi nikue Simple Girl,” kasema.

Aidha, mambo yalichemka pale Simple Boy alipojibu kwa maneno matamu ya kumtoa nyoka pangoni na kumwita Wanja Kihii “Wangu habibi, umenipendeza, uko yomboyombo”.

Mwimbaji huyo wa kibao tajika cha Freshi barida, katika video ya awali alisikika akisema kwamba kwa sasa ametulia na Wanja Kihii na mambo yakiiva atawapakulia uhondo mashabiki wake.

Hili linajiri siku chache baada ya Simple Boy kudai alikuwa anammezea mate msanii Kaveve Kazoze.

Kwa upande mwingine mashabiki mtandaoni wamemchamba Simple Boy.

Blockchain Trader amemwambia Simple Boy “Hii ni mali yangu kimbia”.

Amina Julie amemsuta, akitaka kujua aliko mke halisi wa Simple Boy ambaye walifunga ndoa baada ya kusaidiwa na mbunge Salasya.

“Kwani bibi yake ameenda wapi tena? Akashangaa Harietharriet.

Awali, Simple Boy alikuwa kwenye uhusiano wa kipenzi na mwanasosholaiti Pritty Vishy.

Uhusiano wao ulidumu muda wa miaka mitatu.

 

  • Tags

You can share this post!

Polo alia kama senge lojing’i Murang’a baada ya...

Mkenya aliyefariki katika ajali ya barabara Amerika...

T L