• Nairobi
  • Last Updated April 28th, 2024 4:55 PM
Barcelona wapepeta Mallorca na kupaa hadi nafasi ya pili kwenye jedwali la La Liga

Barcelona wapepeta Mallorca na kupaa hadi nafasi ya pili kwenye jedwali la La Liga

Na MASHIRIKA

BARCELONA walipaa hadi nafasi ya pili kwenye msimamo wa jedwali la Ligi Kuu ya Uhispania (La Liga) baada ya kupokeza Mallorca kichapo cha 2-1 mnamo Jumapili usiku ugani Camp Nou.

Ushindi huo ulikomesha rekodi duni ya Barcelona waliokuwa wamepoteza mechi tatu mfululizo kwenye mashindano yote katika uwanja wao wa nyumbani.

Barcelona hawajahi kupoteza michuano minne mfululizo ugani Camp Nou. Waliwekwa kifua mbele na Memphis Depay katika dakika ya 25 kabla ya Sergio Busquets kuwafungia bao la pili mwanzoni mwa kipindi cha pili. Bao lililofungwa na Depay lilikuwa zao la ushirikiano mkubwa kati yake na beki Jordi Alba.

Mallorca walifutiwa machozi na nahodha Antonio Raillo katika dakika ya 79 baada ya kuandaliwa krosi safi na Salva Sevilla.

Chini ya kocha Xavi Hernandez, Barcelona kwa wanajivunia alama 66 huku pengo la pointi 15 likitamalaki kati yao na Real Madrid ambao tayari wametawazwa mabingwa wa La Liga msimu huu.

Sevilla ambao pia wametandaza jumla ya mechi 34, wanashikilia nafasi ya tatu kwa alama 64, tatu nyuma ya wafalme wa 2020-21, Atletico Madrid wanaofunga orodha ya nne-bora. Mallorca wanakamata nafasi ya 16 kwa pointi 32, sita mbele ya Levante wanaovuta mkia.

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

  • Tags

You can share this post!

Wafanyikazi wanaopata mishahara duni wapewa nyongeza ya...

TAHARIRI: Kuongeza ujira ni sawa, ila uchumi uboreshwe

T L