• Nairobi
  • Last Updated May 4th, 2024 1:14 PM
Benzema aangika daluga za gozi la timu yake ya taifa

Benzema aangika daluga za gozi la timu yake ya taifa

NA MASHIRIKA

PARIS, Ufaransa

MSHAMBULIAJI matata Karim Benzema amestaafu kucheza soka ya kimataifa baada ya hapo awali kujiondoa kwenye kikosi cha Ufaransa kutokana na jeraha pajani alilopata siku moja kabla ya Kombe la Dunia kuanza nchini Qatar.

Baada ya kujumuishwa katika kikosi cha Didier Deschamps kilichoshiriki kwenye Kombe la Dunia, jeraha lilikatiza ndoto ya mshindi huyo wa tuzo ya Ballon d’Or 2022 ya Mchezaji Bora wa Dunia.

Kukosena kwa staa huyo wa klabu ya Real Madrid kulivuruga juhudi za Les Bleus kuhifadhi ubingwa, baada ya kuchapwa na Argentina fainali, Jumapili iliyopita.

Jina la nyota huyo aliyevumilia uhusiano mbaya dhidi ya Deschamps lilibakia kikosini, hata baada ya Ufaransa kufuzu kwa fainali, na wengi walimtarajia kurejea kikosini baada ya kuonekana akifanya mazoezi na klabu yake ya Madrid, lakini kocha Deschamps hakumuita.

Benzema alianza kuchezea Ufaransa kwa mara ya kwanza 2007 na kuwakilisha taifa lake katika mashindano makubwa wakati wa Euro 2008 na 2012, pamoja na Kombe la Dunia la 2014.

Alikosekana kwa kipindi kirefu baada ya kuhusishwa katika ufisadi, kabla ya baadaye kurejea kikosini kwa ya michuano ya Euro 2020, ambayo Ufaransa ilibanduliwa mapema.

Aliisaidia timu hiyo kutwaa ubingwa wa Nations League mwezi Oktoba 2021.

Benzema amestaafua baada ya kuchezea Ufaransa mara 97 na kufunga mabao 37, lakini sasa mwanasoka huyo mwenye umri wa miaka 35 atabakia kusakatia klabu yake ya Real Madrid.

  • Tags

You can share this post!

KCPE: Kaunti za Kwale na Kilifi zawika Pwani

Giza kuhusu nafasi za waume wa magavana

T L