• Nairobi
  • Last Updated May 19th, 2024 9:50 AM
Brentford yaduwaza Arsenal katika mchuano wa ufunguzi wa EPL msimu huu

Brentford yaduwaza Arsenal katika mchuano wa ufunguzi wa EPL msimu huu

Na MASHIRIKA

BRENTFORD walisherehekea marejeo yao katika Ligi Kuu ya Uingereza (EPL) baada ya miaka 74 kwa ushindi wa 2-0 dhidi ya Arsenal katika mchuano wa ufunguzi wa kipute hicho msimu huu usiku wa Ijumaa ugani Community.

Chini ya kocha Thomas Frank, Brentford walimiliki asilimia kubwa ya mpira na kuonekana kuwazidia Arsenal maarifa katika takriban kila idara.

Kikosi hicho kiliwekwa uongozini na Sergi Canos katika dakika ya 22 kabla ya Christian Norgaard kupachika wavuni goli la pili katika dakika ya 73.

Kati ya wanasoka wa Arsenal waliojituma zaidi ugani ni Emile Smith Rowe na Nicolas Pepe waliomfanyia kipa David Raya kazi ya ziada katika kipindi cha pili. Hata hivyo, juhudi zao hazikuzaa matunda yoyote.

Arsenal walikuwa bila mafowadi Alexandre Lacazette na Pierre-Emerick Aubameyang wanaougua. Mads Bech Sorensen alitatiza pakubwa safu ya nyuma ya Arsenal iliyokuwa chini ya ulinzi wa beki Ben White aliyesajiliwa kwa Sh7.8 bilioni kutoka Brighton muhula huu.

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

You can share this post!

Mwanamke ashtakiwa kumdhulumu bintiye

Mwanamme ashtakiwa kutisha kuua mwanamke akiyekataa...