• Nairobi
  • Last Updated May 5th, 2024 7:50 AM
Brentford yaduwaza Man-City katika EPL ugani Etihad

Brentford yaduwaza Man-City katika EPL ugani Etihad

Na MASHIRIKA

MANCHESTER City walipoteza alama nyingine muhimu katika Ligi Kuu ya Uingereza (EPL) msimu huu baada ya Brentford kuwapokeza kichapo cha 2-1 mnamo Jummaosi ugani Etihad.

Mechi hiyo ilikuwa ya pili kwa masogora hao wa Pep Guardiola kupoteza ligini muhula huu baada ya Liverpool kuwacharaza 1-0 mnamo Oktoba 16, 2022 ugani Anfield.

Bao la Brentford dhidi ya Man-City lilijazwa kimiani na Ivan Toney mwishoni mwa kipindi cha pili. Matokeo hayo yalisaza Man-City katika nafasi ya pili kwa alama 32, tisa kuliko Man-United ambao wana mchuano wa akiba. Brentford kwa upande wao wanakamata nafasi ya 10 kwa alama 19 sawa na Crystal Palace na Fulham.

Man-United ambao ni mabingwa mara 20 wa EPL kwa sasa wanajivunia alama 23 kutokana na mechi 13 za ufunguzi wa msimu huu baada ya kushinda michuano saba, kupiga sare mara mbili na kupoteza mapambano manne. Fulham kwa upande wao wamejizolea pointi 19 kutokana na michuano 14.

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

  • Tags

You can share this post!

BAHARI YA MAPENZI: Bosi wa kijakazi mume au mke?

DARUBINI YA WIKI: Toleo Nambari 11 | Novemba 13, 2022

T L