• Nairobi
  • Last Updated May 13th, 2024 10:55 AM
Chipukizi Kimathi ajiuzulu mkondo wa mwisho Croatia Rally

Chipukizi Kimathi ajiuzulu mkondo wa mwisho Croatia Rally

Na GEOFFREY ANENE

DEREVA chipukizi McRae Kimathi na mwelekezi wake Mwangi Kioni hawakuponea ukatili wa mbio za magari Croatia kwenye lami baada ya kusalimu amri katika duru hiyo ya dunia siku ya mwisho hapo Jumapili.

Wakiendesha gari la Ford Fiesta R3, Wakenya hao walikuwa na siku mbili nzuri za kwanza mnamo Aprili 22 na Aprili 23, lakini wakajiuzulu katika mkondo wa 20 (mwisho) katika eneo la Zagorska Sela hadi Kumrovec 2 wa kilomita 14.09.

Katika mikondo yote 19 waliyofanya, nafasi nzuri walikuwa wamekamata ni 43, katika mkondo wa tisa (Kostanjevac-Petrus Vrh 1) na ule wa kumi Jaskovo-Mali Modrus Potok 1) Jumamosi.

Madereva 63 walioanza mashindano hayo ya jumla ya kilomita 1,642.18 ambayo raia wa Finland, Kalle Rovanpera akishirikiana na Jonne Halttunen waliibuka washindi wakipaisha Toyota Yaris R1. Walimaliza sekunde 4.3 mbele ya Ott Tanak/Martin Jarveoja (Hyundai i20 R1).

Kimathi alikuwa Mwafrika wa kwanza kukamilisha duru ya dunia ya Uswidi mwezi Februari. Duru ijayo Kimathi atafanya ni Ureno mnamo Mei 19-22.

  • Tags

You can share this post!

UhuRuto walivyofuta mafanikio ya Kibaki

Rais Kenyatta aongoza Wakenya kuanza kuutazama mwili wa...

T L