Na MASHIRIKA
MASAIBU ya Borussia Dortmund kwenye kampeni za Ligi Kuu ya Ujerumani (Bundesliga) msimu huu yaliendelezwa na SC Freiburg mnamo Jumamosi usiku baada ya kupokezwa kichapo cha 2-1 ugenini.
Jeong Woo-yeong aliwaweka wenyeji Freiburg kifua mbele kunako dakika ya 49 kabla ya Jonathan Schmid kuongeza la pili dakika tatu baada ya kumzidi maarifa kipa Marwin Hitz.
Kiungo mvamizi raia wa Norway, Erling Braut Haaland, alichangia goli lililowarejesha Dortmund mchezoni kupitia kwa chipukizi Youssoufa Moukoko, 16, katika dakika ya 76.
Kusuasua kwa Dortmund kwenye mchuano huo kuliwashusha hadi nafasi ya sita jedwalini kwa alama 32 huku pengo la pointi 16 likitamalaki kati yao na viongozi wa jedwali, Bayern Munich.
Dortmund kwa sasa wanajiandaa kuwaalika Hoffenheim kwa ajili ya gozi la Bundesliga mnamo Februari 13 kabla ya kuwaendea Sevilla ya Uhispania kwenye hatua ya 16-bora ya Klabu Bingwa Ulaya (UEFA) mnamo Februari 17, 2021.
MATOKEO YA Bundesliga (Februari 6):
Freiburg 2-1 Dortmund
Mainz 1-0 Union Berlin
Leverkusen 5-2 Stuttgart
Augsburg 0-2 Wolfsburg
Schalke 0-3 Leipzig
M’gladbach 1-2 FC Koln
TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO