• Nairobi
  • Last Updated May 21st, 2024 10:55 AM
Chombo cha Dortmund chazamishwa tena

Chombo cha Dortmund chazamishwa tena

Na MASHIRIKA

MASAIBU ya Borussia Dortmund kwenye kampeni za Ligi Kuu ya Ujerumani (Bundesliga) msimu huu yaliendelezwa na SC Freiburg mnamo Jumamosi usiku baada ya kupokezwa kichapo cha 2-1 ugenini.

Jeong Woo-yeong aliwaweka wenyeji Freiburg kifua mbele kunako dakika ya 49 kabla ya Jonathan Schmid kuongeza la pili dakika tatu baada ya kumzidi maarifa kipa Marwin Hitz.

Kiungo mvamizi raia wa Norway, Erling Braut Haaland, alichangia goli lililowarejesha Dortmund mchezoni kupitia kwa chipukizi Youssoufa Moukoko, 16, katika dakika ya 76.

Kusuasua kwa Dortmund kwenye mchuano huo kuliwashusha hadi nafasi ya sita jedwalini kwa alama 32 huku pengo la pointi 16 likitamalaki kati yao na viongozi wa jedwali, Bayern Munich.

Dortmund kwa sasa wanajiandaa kuwaalika Hoffenheim kwa ajili ya gozi la Bundesliga mnamo Februari 13 kabla ya kuwaendea Sevilla ya Uhispania kwenye hatua ya 16-bora ya Klabu Bingwa Ulaya (UEFA) mnamo Februari 17, 2021.

MATOKEO YA Bundesliga (Februari 6):

Freiburg 2-1 Dortmund

Mainz 1-0 Union Berlin

Leverkusen 5-2 Stuttgart

Augsburg 0-2 Wolfsburg

Schalke 0-3 Leipzig

M’gladbach 1-2 FC Koln

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

  • Tags

You can share this post!

Ruto awafokea waliopeleka bandari kavu Naivasha

Guinea watuzwa Sh137.5 milioni CHAN 2021