• Nairobi
  • Last Updated May 2nd, 2024 8:55 PM
COVID-19: Mechi za EFL za Disemba 26, 2021 zaahirishwa

COVID-19: Mechi za EFL za Disemba 26, 2021 zaahirishwa

Na MASHIRIKA

MECHI mbili za Ligi ya Daraja ya Kwanza nchini Uingereza (Championship) zilizokuwa zipigwe Disemba 26, 2021 na tano nyinginezo katika Ligi ya Daraja ya Tatu (League Two), zimeahirishwa kwa sababu ya corona.

Gozi lililokuwa likutanishe Cardiff na Coventry kisha kivumbi kati ya Stoke City na Barnsley sasa zitaratibiwa upya.Kwa mujibu wa vinara wa EFL, yapo matumaini kwamba kalenda ya mechi nyingi za msimu huu haitavurugwa sana na michuano mbalimbali ya ligi, Carabao Cup na Papa John’s Trophy itaendelea iwapo itakuwa salama kwa mapambano hayo kuandaliwa.

Viongozi wa Ligi ya Daraja ya Tatu, Forest Green sasa wameshuhudia michuano yao mitatu mfululizo ikiahirishwa na mechi yao nyingine ni kati ya tano ambazo sasa zimeahirishwa tena katika League Two. Forest Green vs Newport, Bristol Rovers vs Sutton, Northampton vs Walsall, Bradford vs Harrogate na Exeter vs Swindon ni miongoni mwa mechi ambazo zimeahirishwa kufikia sasa.

Hizi ni kati ya mechi saba ambazo zimeathiriwa mnamo Disemba 26, 2021.

MECHI ZILIZOAHIRISHWA:

Championship

Barnsley vs Stoke City

Cardiff City vs Coventry City

League Two

Bristol Rovers vs Sutton United

Bradford City vs Harrogate Town

Exeter City vs Swindon Town

Newport County vs Forest Green Rovers

Northampton Town vs Walsall

You can share this post!

Wan-Bissaka atozwa faini na kupigwa marufuku ya kuendesha...

Marudiano kwenye raundi za tatu na nne katika Kombe la FA...

T L