• Nairobi
  • Last Updated May 2nd, 2024 8:55 PM
Everton wapata mfumaji wa kujaza pengo la Richarlson Andrade aliyeyoyomea Tottenham

Everton wapata mfumaji wa kujaza pengo la Richarlson Andrade aliyeyoyomea Tottenham

Na MASHIRIKA

EVERTON wameimarisha safu yao ya mbele baada ya kusajili mvamizi Neal Maupay kutoka Brighton kwa mkataba wa miaka mitatu.

Mfaransa huyo aliyekataa ofa ya kujiunga na Fulham ya mkufunzi Marco Silva, anatua ugani Goodison Park kujaza pengo la fowadi Richarlson Andrade aliyeyoyomea Tottenham Hotspur kwa Sh8.5 bilioni mnamo Julai.

Chini ya kocha Frank Lampard, Everton walisalia bila fowadi tegemeo mwanzoni mwa msimu huu baada ya Dominic Calvert-Lewin kupata jeraha la goti linalotarajiwa kumweka mkekani kwa takriban wiki sita zijazo.

Maupay, 26, alifungia Brighton mabao 26 kutokana na mechi 102 tangu aagane na Brentford waliomwachilia kuondoka kwa Sh2.8 bilioni mnamo 2019.

Anakuwa sogora wa sita kusajiliwa na Everton muhula huu baada ya James Tarkowski, Ruben Vinagre, Dwight McNeil, Conor Coady na Amadou Onana.

Maupay ni sogora wa tatu wa haiba kubwa kuagana na Brighton muhula huu baada ya beki Marc Cucurella kuyoyomea Chelsea kwa Sh8.8 bilioni na kiungo Yves Bissouma kujiunga na Spurs kwa Sh3.6 bilioni.

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

You can share this post!

Pigo kwa Chelsea jeraha likimweka nje nyota tegemeo...

Maguire aambiwa unahodha hautampa uhakika wa kuunga kikosi...

T L