• Nairobi
  • Last Updated May 6th, 2024 8:55 PM
Pigo kwa Chelsea jeraha likimweka nje nyota tegemeo N’Golo Kante kwa wiki nne zijazo

Pigo kwa Chelsea jeraha likimweka nje nyota tegemeo N’Golo Kante kwa wiki nne zijazo

NA MASHIRIKA

KOCHA Thomas Tuchel wa Chelsea amethibitisha kwamba kiungo tegemeo N’Golo Kante sasa atasalia mkekani kuuguza jeraha la paja kwa kipindi cha wiki nne zijazo.

Kante, 31, aliumia wakati wa mechi iliyoshuhudia Chelsea wakilazimishiwa sare ya 2-2 kutoka kwa Tottenham Hotspur uwanjani Stamford Bridge mnamo Agosti 14, 2022. Jeraha hilo lilimweka nje ya pambano jingine la Ligi Kuu ya Uingereza (EPL) ambalo liliwapa Leeds United jukwaa la kutandika Chelsea 3-0 mnamo Agosti 21, 2022 ugani Elland Road.

Chelsea wamekosa huduma za Tuchel wakati wa mechi dhidi ya Leicester City mnamo Agosti 27, 2022 baada ya kuonyeshwa kadi nyekundu kwa kuvurugana na mkufunzi Antonio Conte wa Spurs mwishoni mwa mechi iliyosakatwa mnamo Agosti 14.

Pigo zaidi kwa Chelsea leo pia ni kumkosa pia kiungo matata raia wa Croatia, Mateo Kovacic, ambaye pia anauguza jeraha la goti. Ingawa hivyo wamepiga Leicester 2-1.

Beki Kalidou Koulibaly aliyesajiliwa kutoka Napoli muhula huu, amekosa pia pambano dhidi ya Leicester mnamo Agosti 27, 2022 uwanjani Stamford Bridge baada ya kuonyeshwa kadi nyekundu dhidi ya Leeds.

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

You can share this post!

Kimya kirefu cha Rais chazua hofu kwa Ruto

Everton wapata mfumaji wa kujaza pengo la Richarlson...

T L