• Nairobi
  • Last Updated May 18th, 2024 3:46 PM
Faki, Wanjiru imani wataunga timu ya taifa Hit Squad

Faki, Wanjiru imani wataunga timu ya taifa Hit Squad

Na CHARLES ONGADI

MABONDIA Mwinyi Kombo Faki na Ann Wanjiru wameelezea furaha yao baada ya kushinda mapigano yao kwenye fainali ya Jamal Cup, Kisumu, majuma machache yaliyopita.

Wawili hao, waliowakilisha klabu ya Kongowea ya Mombasa, wamesema wana matumaini makubwa ya kuchaguliwa katika timu ya taifa itakayoshiriki mashindano ya kimataifa mwaka ujao.“ Ushindi wetu Kisumu umekuja wakati mzuri kutokana kwamba ndondi hizo zilitumiwa pia kuchagua timu ya taifa, “ akasema Mwinyi katika mazungumzo na Taifa Leo hapo jana.

Katika fainali yake Mwinyi alimtandika Michael Donga wa Nairobi kwa wingi wa pointi, kwenye uzito wa Bantam. Naye Wanjiru alimzaba Emilly Juma wa Nairobi katika raundi ya tatu uzito wa Fly.Itakuwa ni kuvunja mwiko endapo mabondia hao watakosa kuunga timu ya taifa, almaarufu Hit squad, baada ya kikosi hicho kumilikiwa na mabondia wengi wa Nairobi kwa kipindi kirefu.

Baadhi ya mabondia wa Pwani waliowahi kuwakilisha Kenya kimataifa ni Martin ‘ Nyoka ‘ Ojwang’ uzito wa Middle. Kocha Mkuu Musa Benjamin alisema mabondia watachaguliwa kulingana na ubora wao kwenye mashindano ya Jamal Cup.

You can share this post!

Klabu za NSL zawakia FKF

Kenya yapigia debe Tong-IL Moo-Do iwepo katika Olimpiki za...

T L