• Nairobi
  • Last Updated May 13th, 2024 6:29 PM
Franck Ribery ajiunga na Salernitana ya Italia akiwa na umri wa miaka 38

Franck Ribery ajiunga na Salernitana ya Italia akiwa na umri wa miaka 38

Na MASHIRIKA

NYOTA wa zamani wa timu ya taifa ya Ufaransa na klabu ya Bayern Munich, Franck Ribery, 38, amejiunga na kikosi cha Salernitana kilichopandishwa ngazi mwishoni mwa msimu wa 2020-21 kushiriki Ligi Kuu ya Italia (Serie A).

Ribery anaingia katika sajili rasmi ya Salernitana baada ya kuagana na Fiorentina mwishoni mwa msimu uliopita.

Fowadi huyo veterani alinyanyua mataji tisa ya Ligi Kuu ya Ujerumani (Bundesliga) na ufalme wa Klabu Bingwa Ulaya (UEFA) katika kipindi cha miaka 12 ya kuhudumu kwake kambini mwa Bayern.

Ribery alikuwa akihusishwa na uwezekano mkubwa wa kurejea Bayern kwa matarajio ya kuwa kocha wa miamba hao wa Ujerumani katika siku za usoni.

Ribery aliwajibishwa na timu ya taifa ya Ufaransa mara 81 na alikuwa sehemu ya kikosi kilichotinga fainali ya Kombe la Dunia mnamo 2006.

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO 

You can share this post!

CBC yalemea wazazi

Wamalwa ahimiza viongozi wa OKA wasiwe na ubinafsi