• Nairobi
  • Last Updated May 4th, 2024 7:55 AM
Fulham wasajili kipa Bernd Leno kutoka Arsenal

Fulham wasajili kipa Bernd Leno kutoka Arsenal

Na MASHIRIKA

FULHAM wamemsajili kipa raia wa Ujerumani, Bernd Leno kutoka Arsenal kwa mkataba wa miaka mitatu uliogharimu kima cha Sh1.1 bilioni.

Leno, 30, alipoteza nafasi yake katika kikosi cha kwanza cha Arsenal mnamo 2021-22 ambapo aliwajibishwa mara tisa pekee baada ya kikosi hicho cha kocha Mikel Arteta kujinasia maarifa ya Aaron Ramsdale.

Katika mechi zote 125 ambazo Leno alichezea Arsenal, hakufungwa katika michuano 37 pekee tangu asajiliwe kutoka Bayer Leverkusen ya Ujerumani kwa Sh2.9 bilioni mnamo 2018.

Leno anakuwa mchezaji wa tano kusajiliwa na Fulham tangu warejee kwenye Ligi Kuu ya Uingereza (EPL). Wachezaji wengine wapya ugani Craven Cottage ni Joao Palhinha, Andreas Pereira, Kevin Mbabu na Manor Solomon.

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

  • Tags

You can share this post!

Sonko ahemesha Omar kampeni za kusaka ugavana

Meneja wa New KPCU ataja mikakati yake ya kukabili wizi wa...

T L