• Nairobi
  • Last Updated May 6th, 2024 10:55 AM
Gor na Leopards mashakani

Gor na Leopards mashakani

Na JOHN ASHIHUNDU

MABINGWA wa ligi kuu nchini, Gor Mahia na mahasimu wao wakuu, AFC Leopards huenda wakajipata mashakani kutokana na madeni wanayodaiwa na wachezaji wao wa zamani.

Tayari timu hizo kongwe zimepigwa marufuku kusajili kwa misimu miwili ijayo kwa kushindwa kulipa Dickson Ambundo na Vincent Habamahahoro mtawaliwa.

Akitoa habari hizo, Wakili Evans Majani alidai kwamba huenda klabu hizo zikateremshwa ngazi kwa kushindwa kulipa madeni hayo ya Sh3 milioni kwa jumla.

Ambundo anaidai Gor Mahia Sh1.2 milioni wakati Habamahahoro akiidai Leopards Sh1.8 milioni.

Majani alisema Fifa iliafikia uamuzi huo mwezi uliopita baada ya klabu hizo kupuuza agizo la Mahakama ya Kutatua Mizozo Michezoni (DRC).

“Iwapo wataendelea kupuuza agizo hili, tutalazimika kuandikia DRC kutafuta usaidizi wao na vikwazo zaidi ambavyo ni pamoja na kushusha timu hizo hadi daraja la chini,” aliongeza.

Majani alisema Wazito FC wamemlipa Issofou Bourhana na Augustine Otu na Piscas Kirenge, lakini wanadaiwa na Paul Acquah na Mansoor Safi Agu.

“Iwapo Gor Mahia na Leopards zitaendelea kutuzungusha, tutarejea kwa Fifa kwa hatua zaidi dhidi yao. Lazima walipe kwa sababu waliwatimua wachezaji hao ghafla,” alisema Majani.

Habari hizo zimetokea siku chache tu baada ya mlinzi Moussa Omar raia wa Burundi kusisitiza kwamba anataka Sofapaka imelipe Sh1 milioni kwa kumuachisha kazi ghafla mnamo 2019.

Akizungmza kuhusu tukio hilo, Maneja Mtendaji wa Sofapaka, Jimmy Ambajo alisema tayari wamezungmza na Omar kumtaka atulie hadi pesa zitakapopatikana. Alisema huenda wakamlipa kufikia Agoisti 2021.

You can share this post!

Ombi la kuchangishia shujaa Ayimba ambaye ni mgonjwa Sh2...

Mhubiri Nyeri achoma karatasi za kutangaza huduma za waganga