• Nairobi
  • Last Updated May 18th, 2024 6:09 PM
Juventus yaadhibu AS Roma ya kocha Jose Mourinho kwenye gozi la Serie A

Juventus yaadhibu AS Roma ya kocha Jose Mourinho kwenye gozi la Serie A

Na MASHIRIKA

MOISE Kean alifunga bao la pekee na la ushindi katika mechi iliyoshuhudia Juventus wakipepeta AS Roma ya kocha Jose Mourinho katika Ligi Kuu ya Italia (Serie A).

Ushindi huo ulikuwa wan ne mfululizo kwa Juventus ya kocha Massimiliano Allegri kusajili katika Serie A.

Kean anayechezea Juventus kwa mkopo kutoka Everton alifunga bao la waajiri wake kwa sasa katika dakika ya 16 baada ya kombora lake kumbabatiza beki Rodrigo Bentancur wa Roma.

Roma walipata fursa ya kusawazisha mwishoni mwa kipindi cha kwanza ila penalti ya Jordan Veretout iliyotokana na tukio la Tammy Abraham kuchezewa visivyo ndani ya kijisanduku ikapanguliwa na kipa Wojciech Szczesny.

Ingawa Abraham alikuwa amejaza mpira wavuni mwa Juventus, refa Daniele Orsata alikuwa tayari amepuliza kipenga cha kuashiria kupigwa kwa penalti.

Japo Abraham aliokota mpira huo kwa nia ya kuchanja penalti hiyo mwenyewe, alipokonywa mpira na Veretout ambaye baadaye alishindwa ujanja na Szczesny.

Nusura Juventus wafunge bao la pili kupitia kwa Federico Bernardeschi mwishoni mwa kipindi cha pili ila juhudi zake zikazimwa na kipa Rui Patricio.

Kichapo ambacho Roma walipokezwa kilikuwa chao cha tatu msimu huu na kwa sasa wanashikilia nafasi ya nne jedwalini kwa alama 15, tisa nyuma ya Napoli wanaoselelea kileleni mwa jedwali.

Matokeo ya Serie A (Oktoba 17, 2021):

Juventus 1-0 AS Roma

Cagliari 3-1 Sampdoria

Empoli 1-4 Atalanta

Genoa 2-2 Sassuolo

Udinese 1-1 Bologna

Napoli 1-0 Torino

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

  • Tags

You can share this post!

Uhuru adokeza kuwa huenda akaondoa kafyu

Wachungaji waomba amani idumu Kenya inapojiandaa kwa...

T L