• Nairobi
  • Last Updated May 9th, 2024 6:50 AM
Kakamega yanasa 3, yataka moja ikafunge

Kakamega yanasa 3, yataka moja ikafunge

Na JOHN KIMWERE

KAKAMEGA Homeboyz imetwaa huduma za wachezaji watatu huku Thomas Wainaina akihamia FC Talanta kwa maelewano kutoka pande zote mbili.

Kocha wa Kakamega, Bernard Mwalala amethibitisha kuwa beki huyo amehama baada ya Evans Maliachi kujiunga na klabu hiyo akitokea FC Talanta ya kocha Ken Kenyatta. ”Sio duru tena ni kweli kuwa mchana nyavu huyo aliyewahi kuchezea Sofapaka FC, Nzoia Sugar na Nakuru All Stars amehamia FC Talanta kulingana na mazungumzo ya timu zote mbili.

Ni mchezaji mzuri na bila shaka namtakia kila la heri katika klabu yake pia taaluma yake ya soka inakoamini ataendelea kufanya vizuri,” Mwalala alisema. Kando na Evans Maliachi Kakamega inayoongoza katika jedwali la Ligi Kuu ya Shirikisho la Soka la Kenya (FKF-PL) imesajili Mike Isabwa kutoka Vihiga Bullets na Gaetan Masha akitokea Nzoia Sugar.

”Tunataka kusajili kiungo mmoja na tukafunge maana nafasi hiyo inahitaji kupigwa jeki,” akasema na kuongeza kuwa pia wanao wachezaji chipukizi wengi wanaopania kuwaachia kwa mikopo ili wapate nafasi za kucheza baada ya kukaa benchi kwa muda.

Kwenye ratiba ya kipute hicho Kakamega Homeboyz inayozidi kufanya kweli imepangwa kucheza na Nzoia Sugar FC wiki hii. Katika msimamo wa kinyang’anyiro hicho, Kakamega ingali kifua mbele kwa kuzoa alama 33, nne mbele ya KCB.

Kariobangi inafunga tatu bora kwa kusajili pointi 28 sawa na City Stars maarufu Nairobi Simba tofauti ikiwa idadi ya mabao huku Gor Mahia ikifunga tano bora kwa alama 27

You can share this post!

Mudavadi afichua sababu ya kugura OKA

Wito polisi wajengewe vituo vya ushauri nasaha

T L