• Nairobi
  • Last Updated May 18th, 2024 10:55 AM
Kibera Girls kifua mbele ligi ya taifa daraja la kwanza

Kibera Girls kifua mbele ligi ya taifa daraja la kwanza

Na JOHN KIMWERE

KOCHA wa Kibera Girls Soccer, Davis Ikochela amesema wamepania kuendeleza mtindo wa kugawa dozi dhidi ya wapinzani wao kwenye mechi za Kundi A Ligi ya Taifa Daraja la Kwanza.

Amedokeza hayo baada ya kusajili ushindi wa magoli 3-1 mbele ya Soccer Sisters wikendi. ”Ninaamini wachezaji wangu wamekaa vizuri kufanya kweli kwenye kampeni za muhula huu,” alisema na kuwataka kuwa makini kwenye mechi zijazo.

Aidha amesema kuwa lazima wapambane kiume kuwania tiketi ya kufuzu kupandishwa ngazi kurejea kushiriki mechi za Ligi Kuu ya Soka la Wanawake (KWPL) msimu ujao. Kwenye mchezo huo vipusa hao waling’ata wapinzani wao kupitia Pauline Atieno aliyetikisa wavu mara mbili naye Pauline Akinyi alifunga goli moja.

Kufuatia matokeo hayo Kibera Girls Soccer ingali kileleni mwa jedwali kwa kuzoa alama kumi, tatu mbele ya Mathare Women FC iliyotoka sare tasa dhidi ya MTG United. Ivy Zarah alifungia Soccer Sisters bao la kufutia machozi. Nayo Uweza Women ilikung’uta Limuru Starlets mabao 2-1 na kufunga tano bora kwa alama nne sawa na Sunderland Samba tofauti ikiwa idadi ya mabao.

Uweza ilipata ufanisi huo kupitia juhudi za Marion Andesia na Mercy Mwachi waliofunga bao moja kila mmoja. Makolanders ilitoka nguvu sawa mabao 4-4 na Mombasa Olympic huku Noel Makokha akicheka na wavu mara moja na kubeba Oserian Ladies kuzoa bao 1-0 mbele ya Solasa Stima Queens.

You can share this post!

LEAP2022: Saudi Arabia yazindua uwekezaji wa Sh700 bilioni...

Kocha Harambee Starlets kibarua kuteua timu ya mwisho

T L