• Nairobi
  • Last Updated May 14th, 2024 7:55 AM
Kitaumana leo Etihad

Kitaumana leo Etihad

MANCHESTER, ?Uingereza

Na MASHIRIKA

MANCHESTER City wataingia uwanjani Etihad kwa lengo moja kuu; kulipiza kisasi dhidi ya Paris Saint-Germain (PSG) ya Ufaransa katika pambano la Klabu Bingwa Ulaya (UEFA), hatua ya makundi leo usiku

Kwenye mechi ya mkondo wa kwanza iliyochezewa Parc de Princes mjini Paris, PSG – ambao wanashikilia nafasi ya pili kwenye kundi hilo la A – waliibuka washindi kwa mabao 2-0 dhidi ya vinara Man-City.

Masogora wa Guardiola waliwanyuka Club Bruges 4-1 ugenini nchini Ubelgiji na kutua kileleni mwa kundi.Matokeo hayo yaliiwezesha City kuongoza kundi hilo baada ya PSG kutoka sare na RB Leipzig katika pambano jingine.

Katika mechi ya leo, kocha Guardiola anatarajiwa kupanga kikosi cha kupata ushindi, utakaowawezesha kumaliza mechi za makundi wakiwa wamenata katika nafasi hiyo ya kwanza.

Guardiola hajawahi kushinda kombe la UEFA akiinoa Manchester City, na wengi wanadhania wakati huo umewadia msimu huu.City wanaingia dimbani wakijivunia ushindi mara nane mfululizo katika uwanja wao wa nyumbani kwenye michuano hii ya Ulaya.

Lakini PSG wanacheza pambano la leo wakati staa Lionel Messi ameanza kuonyesha makali yake tangu ajiunge nao.Matumaini ya PSG kumaliza katika nafasi ya kwanza kundini yalivurugwa kufuatia sare ya 2-2 dhidi ya RB Leipzig, na sasa wako nyuma ya Man-City kwa mwanya wa pointi moja baada ya kucheza mechi tatu bila kushindwa.

Liverpool, ambao tayari wamefuzu kwa hatua ya 16-bora, watakuwa nyumbani kuvaana na FC Porto katika mechi ya Kundi B.Ugani Anfield, wenyeji Liverpool chini ya kocha Jurgen Klopp wataingia dimbani wakijivunia pointi 12 kutokana na mechi nne.Nao Porto, wanaokamata nafasi ya pili kundini, wako na alama tano.

Liverpool wametinga hatua ijayo ya muondoano wakiwa wamebakisha mechi mbili kundini, kufuatia ushindi wa 2-0 dhidi ya Atletico Madrid mapema mwezi huu.Nyumbani Anfield wamesakata mechi 14 bila kushindwa msimu huu, lakini haitakuwa kazi rahisi mbele ya Porto ambao watapigania ushindi kwa vyovyote vile.

Liverpool wamekuwa wakifunga angalau mabao mawili katika mechi 15 za karibuni kwenye michuano hii ya UEFA.Henda Klopp akaamua kuwapa nafasi vijana kadhaa ambao wamekuwa katika kikosi cha akiba.

You can share this post!

Tim Wanyonyi Ngamia One FC, City Park zaanza vyema

Voliboli: Tupo ng’ang’ari kutetea taji letu...

T L