• Nairobi
  • Last Updated May 18th, 2024 8:57 PM
Kiungo Idrissa Gueye arejea Everton baada ya kuagana na PSG

Kiungo Idrissa Gueye arejea Everton baada ya kuagana na PSG

Na MASHIRIKA

EVERTON wamemsajili upya kiungo Idrissa Gueye kutoka Paris Saint-Germain (PSG) kwa mkataba wa miaka miwili uliogharimu Sh286 milioni.

Everton wamekuwa wakijitahidi kumrejesha Gueye, 32, ugani Goodison Park tangu mwanzo wa Agosti 2022. Gueye amejiunga upya na Everton saa chache baada ya kikosi hicho kumsajili pia kiungo James Garner, 21, kutoka Manchester United kwa Sh1.3 bilioni.

Gueye aliibuka mchezaji bora wa Everton mnamo 2019 kabla ya PSG kujinasia huduma zake kwa Sh4.3 bilioni. Ada ya kusajiliwa kwa Garner inatarajiwa kuongezeka hadi kufikia Sh2.1 bilioni. Sogora huyo ndiye mchezaji wa nane kusajiliwa na Everton muhula huu baada ya kuhudumu kambini mwa Nottingham Forest kwa mkopo.

Garner alikuwa tegemeo kubwa la Forest waliotinga robo-fainali za Kombe la FA Cup na akarejea EPL baada ya miaka 23 ambapo aliwajibishwa mara 49 na akapachika wavuni mabao manne.

Gueye alifungia PSG mabao saba pekee kutokana na mechi 111 na akaongoza miamba hao kushinda Ligi Kuu ya Ufaransa (Ligue 1) mara mbili na ubingwa wa French Cup mara mbili kisha kuwaongoza waajiri wake kufuzu kwa fainali ya Klabu Bingwa Ulaya (UEFA) mnamo 2020.

 TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

  • Tags

You can share this post!

Wanne wamezea mate uspika Kaunti ya Kisumu

Ruto na Chebukati wajibu makombora

T L