• Nairobi
  • Last Updated May 4th, 2024 10:15 PM
Kiungo wa Brazil, Allan, aondoka Everton na kuyoyomea UAE kuvalia jezi za Al-Wahda

Kiungo wa Brazil, Allan, aondoka Everton na kuyoyomea UAE kuvalia jezi za Al-Wahda

Na MASHIRIKA

KIUNGO wa zamani wa Brazil, Allan, 31, ameondoka kambini mwa Everton na kujiunga na kikosi cha Al-Wahda cha United Arab Emirates ambacho kimemsajili kwa mkataba wa miaka miwili.

Allan alijiunga na Everton kwa kima cha Sh3 bilioni baada ya kuagana na Napoli ya Ligi Kuu ya Italia (Serie A) mnamo 2020.

Ingawa alisakata mechi 52 za Ligi Kuu ya Uingereza (EPL) katika misimu yake miwili ya kwanza, hakuchezeshwa katika pambano lolote la kivumbi hicho mnamo 2022-23.

Chini ya kocha Frank Lampard, Everton wameimarisha safu yao ya kati muhula huu kwa kujinasia huduma za nyota Idrissa Gueye na Amadou Onana.

Al Wahda kwa sasa wananolewa na kocha wa zamani wa Swansea City na Sheffield Wednesday, Carlos Carvalhal. Kiungo wa zamani wa Leicester City, Adrien Silva, ni miongoni mwa wanasoka tegemeo kambini mwa kikosi hicho.

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

  • Tags

You can share this post!

Richarlson aongoza Brazil kupepeta Ghana katika mechi ya...

Ruto aita wahubiri ikulu kwa maombi

T L