NAIROBI
Na PATRICK KILAVUKA
Kocha wa Leads United Wistone Issa alisema ana furaha mzomzo kutokana na kuanza Ligi ya Kitaifa Daraja ya Pili kwa matao baada ya kubwaga Limuru 1-0 katika mchuano ulioandaliwa uga wa Kihumbuini, Jumapili.
“Japo timu ndio ilikuwa imerejelea mazoezi, nilifurahia ushindi huo. Hata hivyo, wapinzani walikuwa wagumu hususan kipindi cha pili waliidhibiti timu sana. Kwa sasa vijana wanaenda kuimarisha mazoezi tukilenga sasa Ligi ya Kitaifa Daraja ya Kwanza,” alisema kocha huyo.
Aidha, mkufunzi wa Olympic Jeremiah Otieno alikiri kwamba japo walishindwa, timu ilikosa uwepo wa wachezaji mihimili watano kwa sababu ya kikazi na bahati hakuwalenga kwani walipoteza nafasi nyingi ambazo zingewazolea ushindi au kufuta goli lililofungwa.
Bao ambalo lilizimisha matumaini ya Olympic lilifungwa na Herman Ngala katika dakika ya nane.