• Nairobi
  • Last Updated May 17th, 2024 11:53 AM
Koth Biro: Patashika sita kupigwa wikendi hii

Koth Biro: Patashika sita kupigwa wikendi hii

Na JOHN KIMWERE

JUMLA ya mechi sita zimepangwa kuchezwa wikendi hii kwenye mfululizo wa kampeni za kuwania taji la Koth Biro makala ya mwaka 2021/2022.

Leads United inayojivunia kubeba taji la Tim Wanyonyi Super Cup 2021 ambayo imepangwa Kundi H itashuka dimbani kukabili Digo United ugani Umeme Ziwani, Nairobi. ”Bila shaka tumepania kujituma kama kawaida ili kuzoa alama zote tatu na kujiongezea tumaini la kusonga mbele,” kocha wa Leads, Winston Isa alisema na kuongeza kuwa nyakati zote nia yao huwa wanalenga kufanya kweli hadi kushiriki fainali.

Katika ratiba hiyo, Kundi A Kisima FC itachuana na Kayole Youth huku kila moja ikiwinda pointi tatu muhimu ili kujiweka pazuri kufuzu kwa robo fainali. Ruaraka Allstars ambayo imepangwa Kundi E ikigaragazana na Kajiado Allstars.

Kwenye mechi za kesho Kundi B, Kayaba FC itapepetana na Ngara United, nayo Rongai United itacheza na Huruma Kona kwenye mechi za Kundi F huku Slumscores ikikutanishwa na Juakali FC. Juakali itacheza mchezo huo siku mbili baada ya kudungwa mabao 2-1 na Huruma Kona.

Kwenye matokeo ya mechi hizo zilizopigwa Alhamisi, Dandora FC ilikomoa Kinsan FC kwa mabao 8-0 kupitia Teddy Sewe aliyepiga kombora mbili. Mengine walifungwa na Samuel Mbaga, Edward Omondi, Faisal Kadir, Maxwell Mboya, Tiron Kariuki na James Osaha. Naye Ramadhan Otieno alitikisa wavu mara moja na kubeba Borussia FC kuzoa ushindi wa bao 1-0 mbele ya Mlango United.

You can share this post!

Kivumbi kushushwa fainali KJ Super Cup

Maafisa wa kufufua kiwanda cha sukari cha Mumias kutoka...

T L