• Nairobi
  • Last Updated May 18th, 2024 10:55 AM
KU yalenga fainali ya Super Cup

KU yalenga fainali ya Super Cup

Na JOHN KIMWERE

KOCHA wa timu ya wanaume ya Chuo Kikuu cha Kenyatta (KU), Victor Luvale anakiri kuwa wanatarajia mtihani mgumu kwenye shindano la Super Cup.

Hata hivyo anashilikia kuwa wamepania kujituma kwa udi na uvumba wakilenga  asema wamepania kutinga nusu fainali kwenye kidumbwedumbwe hicho. KU itashiriki kipute hicho baada ya kuibuka ya sita katika jedwali ya Ligi Kuu msimu uliyopita.

”Tumepania kupambana  kiume kwenye mechi hizo tukaocheza na miamba wa handiboli nchini ikiwamo Black Mamba na Halmashauri ya Nafaka na Mazao nchini (NCPB),”  alisema na kuongeza kamwe hawana hofu bali wanaamini wanaweza.

Itakuwa mara ya pili KU kushiriki kipute hicho tangia mwaka 2014. Kocha huyo anadokeza kuwa wanaendelea na maandalizi kujiweka tayari kwa kipute hicho. Katika ratiba ya michuano hiyo KU imepangwa Kundi B linalojumuisha Kenya General Service Unit (GSU) na Chuo cha Strathmore.

Nalo Kundi A linashikisha Jeshi la Ulinzi (KDF), Black Mamba na NCPB. KU itafungua kampeni zake dhidi ya Strathmore kisha itakutanishwa na GSU.

KU inajivunia wachezaji kadhaa akiwamo Samuel Katuva (nahodha), naibu wake Morgan Simiyu, Dickson Wanyama, Fresnel Khisa, Amos Keter na Isaac Nyongesa.

  • Tags

You can share this post!

Balozi wa Kenya nchini Nigeria Dkt Wilfred Machage afariki

Alenga kutetemesha anga za uigizaji licha ya masaibu

T L