Na MASHIRIKA
BARCELONA walisajili ushindi wa pili mfululizo katika Ligi Kuu ya Uhispania (La Liga) baada ya kukomoa Real Valladolid 4-0 mnamo Jumapili usiku ugani Camp Nou.
Robert Lewandowski alipachika wavuni mabao mawili katika ushindi huo uliowapaisha hadi nafasi ya tatu jedwalini kwa alama saba saw ana Villarreal.
Mabao mengine ya Barcelona wanaotiwa makali na mkufunzi Xavi Hernandez yalifumwa wavuni na Pedri na Sergi Roberto. Barcelona walitamalaki mchezo kwa kipindi kirefu huku wakizidi ujanja kikosi cha Valladolid katika takriban kila idara.
Ushirikiano kati ya Lewandowski na Raphinha Belloli ambaye pia ni sajili mpya wa Barcelona, ulitatiza pakubwa safu ya nyuma ya Valladolid ambao kwa sasa wanakamata nafasi ya 19 jedwalini kwa alama moja kutokana na mechi tatu.
MATOKEO YA LA LIGA (Jumapili):
Barcelona 4-0 Real Valladolid
Espanyol 1-3 Real Madrid
Getafe 0-0 Villarreal
TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO