• Nairobi
  • Last Updated May 9th, 2024 6:40 PM
Lionel Messi aongoza PSG kuzamisha Lyon katika Ligi Kuu ya Ufaransa

Lionel Messi aongoza PSG kuzamisha Lyon katika Ligi Kuu ya Ufaransa

Na MASHIRIKA

LIONEL Messi alifungia Paris Saint-Germain (PSG) bao la pekee na la ushindi dhidi ya Olympique Lyon katika pambano la Ligi Kuu ya Ufaransa (Ligue 1) mnamo Jumapili usiku ugani Groupama.

Matokeo hayo yaliendeleza rekodi nzuri ya kutoshindwa kwa PSG ligini hadi kufikia sasa msimu huu. Kikosi hicho cha kocha Christophe Galtier kinadhibiti kilele cha jedwali la Ligue 1 kwa alama 22, mbili zaidi kuliko Olympique Marseille ambao pia hawajapoteza mechi yoyote msimu huu.

Messi alicheka na nyavu za Lyon katika dakika ya tano baada ya kushirikiana vilivyo na Neymar aliyechangia bao la tano kambini mwa PSG muhula huu. Goli la Messi lilikuwa lake la sita katika mashindano yote ambayo yametandazwa na kikosi cha PSG msimu huu.

Bao la beki Sergio Ramos mwishoni mwa kipindi cha pili halikuhesabiwa na refa baada ya kubainika kwamba alikuwa ameotea Messi alipochanja mpira wa ikabu.

MATOKEO YA LIGUE 1 (Jumapili):

Nice 0-1 Angers

Lyon 0-1 PSG

Reims 0-3 Monaco

Brest 0-1 Ajaccio

Clermont 1-3 Troyes

Marseille 1-1 Rennes

Nantes 0-0 Lens

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO 

  • Tags

You can share this post!

MWALIMU WA WIKI: Makau ni mwalimu stadi na mwandishi

Gachagua adai hana chuki binafsi na Uhuru

T L