• Nairobi
  • Last Updated April 27th, 2024 9:35 PM
Gachagua adai hana chuki binafsi na Uhuru

Gachagua adai hana chuki binafsi na Uhuru

NA SAMMY WAWERU

NAIBU Rais Rigathi Gachagua amesema wazi kwamba hana chuki binafsi na Rais mstaafu, Uhuru Kenyatta.

Bw Gachagua amesema hana uadui wowote na Rais huyo wa nne, aliyestaafu Septemba 13, 2022 na kumpisha mrithi wake Dkt William Samoei Ruto.

Naibu Rais alisema kwamba tofauti zao zilikuwa za kisiasa pekee.

Gachagua aidha alisema yeye na Rais Kenyatta ni marafiki wa tangu jadi.

“Sisi ni marafiki wa karibu. Hatuna uadui wowote. Yaliyojiri yalikuwa tofauti za kisiasa,” akasema.

Alitoa matamshi hayo Jumapili usiku, katika mahojiano na runinga ya NTV.

“Siasa zina kutofautiana kisera… Mambo yakitulia, nitamtafuta turidhie kikombe cha chai,” Naibu wa Rais akaelezea.

Dkt Ruto na yeye baada ya kuapishwa rasmi juma lililopita katika uwanja wa Moi, Kasarani kama Rais na Naibu Rais mtawalia, Bw Gachagua alionekana katika hotuba yake ya kwanza kumshambulia Kenyatta hadharani katika hafla iliyohudhuriwa na viongozi mashuhuri na marais kutoka nchi mbalimbali.

Alidai baadhi ya maafisa katika serikali ya Rais Kenyatta walitumia mamlaka vibaya, na kuhangaisha waliotofautiana naye.

Isitoshe, alidai serikali ya Jubilee imehujumu uchumi, Kenya Kwanza ikiwa na kibarua kigumu kuuinua kutoka ‘sufuri’.

Wandani wa Rais Kenyatta hata hivyo wametofautiana na Gachagua, wakisema kauli yake haina ukweli.

  • Tags

You can share this post!

Lionel Messi aongoza PSG kuzamisha Lyon katika Ligi Kuu ya...

Gachagua aingia Harambee House Annex kwa kicheko na tabasamu

T L