• Nairobi
  • Last Updated May 13th, 2024 2:11 PM
Liverpool kucheza mechi mbili katika wiki ya mwisho kwenye kampeni za msimu huu

Liverpool kucheza mechi mbili katika wiki ya mwisho kwenye kampeni za msimu huu

Na MASHIRIKA

LIVERPOOL watachezea mara mbili katika wiki ya mwisho kwenye kampeni za Ligi Kuu ya Uingereza (EPL) msimu huu baada ya michuano yao kuratibiwa upya.

Chini ya kocha Jurgen Klopp, miamba hao wanaofukuzia jumla ya mataji manne msimu huu, sasa watakuwa wageni wa Southampton uwanjani St Mary’s mnamo Mei 17, siku tatu baada ya kuvaana na Chelsea kwenye fainali ya Kombe la FA.

Mabingwa hao mara 19 wa EPL watafunga rasmi kampeni za muhula huu dhidi ya Wolves ugani Anfield mnamo Mei 22.

Washindani wao wakuu ligini, Manchester City wataonana na West Ham United ugani London Stadium mnamo Mei 15 kabla ya kutamatisha kampeni zao muhula huu dhidi ya Aston Villa ugani Etihad mnamo Mei 22.

Kwa mujibu wa ratiba mpya ya EPL, Man-City watavaana na Wolves uwanjani Molineux mnamo Mei 11. Ina maana kwamba mabingwa hao watetezi wa EPL watatandaza michuano mitatu ligini chini ya kipindi cha siku saba.

Mechi kati ya Liverpool na Southampton ilipanguliwa upya baada ya masogora hao wa Klopp kufuzu kwa fainali ya Kombe la FA uwanjani Wembley mnamo Mei 14, 2022.

Kufikia sasa, Liverpool ambao tayari wameshinda Carabao Cup wanashikilia nafasi ya pili kwenye EPL kwa alama 79, moja nyuma ya viongozi Man-City. Zimesalia mechi tano pekee kabla ya kipenga cha kuashiria mwisho wa msimu huu kutamatika rasmi.

Vikosi vyote hivyo viwili bado vinafukuzia taji la Klabu Bingwa Ulaya (UEFA) huku fainali ikipangiwa kufanyika Mei 28, 2022 jijini Paris, Ufaransa.

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

  • Tags

You can share this post!

Orengo awashauri wanasiasa kuingia katika miungano kwa...

Kibaki alinisaidia kutoka uhamishoni Uganda, Rwanda –...

T L