• Nairobi
  • Last Updated May 18th, 2024 6:09 PM
Liverpool wajinyanyua na kutandika Ajax 2-1 katika UEFA ugani Anfield

Liverpool wajinyanyua na kutandika Ajax 2-1 katika UEFA ugani Anfield

Na MASHIRIKA

BAO la dakika za mwisho wa mchezo kutoka kwa beki Joel Matip liliwapa Liverpool ushindi wa 2-1 dhidi ya Ajax ya Uholanzi mnamo Jumanne usiku ugani Anfield. Ushindi huo ulikwa wa kwanza kwa Liverpool kusajili katika soka ya Klabu Bingwa Ulaya (UEFA) msimu huu.

Kocha Jurgen Klopp aliwaongoza masogora wake kushuka dimbani akiwataka kuweka kutia kapuni alama tatu muhimu ili kufuta aibu ya kudhalilishwa na Napoli 4-1 katika pambano la awali la Kundi A kwenye UEFA.

Liverpool walianza mchuano kwa matao ya juu na wakapata bao la kwanza kupitia kwa Mohamed Salah aliyekamilisha krosi ya Diogo Jota katika dakika ya 17.

Hata hivyo, juhudi zake zilifutwa na Mohammed Kudus aliyesawazishia Ajax katika dakika ya 27 kabla ya Matip kucheka na nyavu za wageni wao kunako dakika ya 89.

Daley Blind alipoteza nafasi kadhaa za wazi za kusawazishia Ajax mwishoni mwa kipindi cha pili kabla ya Matip kuzamisha chombo cha miamba hao wa Uholanzi. Mechi dhidi ya Liverpool ilikuwa ya kwanza baada ya miaka tisa kwa Blind kunogesha katika UEFA.

Ajax waliofungua kampeni za Kundi A kwenye UEFA kwa ushindi wa 4-0 dhidi ya Rangers kutoka Scotland, sasa wanajivunia alama tatu kundini sawa na Liverpool na Napoli ambao wametandaza mchuano mmoja pekee.

Kichapo cha 4-1 ambacho Liverpool walipokezwa na Napoli ya Italia 4-1 ugani Diego Armando Maradona mnamo Septemba 7, 2022 ni matokeo yaliyoendeleza masaibu ya vijana hao wa kocha Klopp.

Hadi walipovaana na Ajax, Liverpool walikuwa wameshinda mechi mbili, kutoka sare mara tatu na kupoteza mchuano mmoja kati ya sita iliyopita katika Ligi Kuu ya Uingereza (EPL).

Sasa wanajivunia nafuu ya kushinda mechi tatu zilizopita ugani Anfield na rekodi ya kutowahi kufungua kampeni za UEFA kwa vichapo viwili mfululizo. Liverpool hawajawahi kupoteza mechi katika uwanja wao wa nyumbani tangu Machi 2022 walipozabwa na Inter 1-0 katika marudiano ya hatua ya 16-bora ya UEFA.

MATOKEO YA UEFA (Jumanne):

Sporting 2-0 Tottenham

Liverpool 2-1 Ajax

Bayern 2-0 Barcelona

Viktoria Plzen 0-2 Inter Milan

Leverkusen 2-0 Atletico Madrid

FC Porto 0-4 Club Bruges

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

  • Tags

You can share this post!

Bayern Munich wakomoa Barcelona katika gozi la UEFA

Magavana Nassir na Barasa wanaapishwa leo

T L