• Nairobi
  • Last Updated May 17th, 2024 6:50 AM
Lukaku akiri kutofurahia maisha Chelsea, adokeza uwezekano wa kurejea Inter Milan

Lukaku akiri kutofurahia maisha Chelsea, adokeza uwezekano wa kurejea Inter Milan

Na MASHIRIKA

MSHAMBULIAJI Romelu Lukaku aliyerejea Chelsea kwa kima cha Sh15.2 bilioni mnamo Agosti 2021 amedokeza uwezekano wa kurejea kambini mwa Inter Milan ya Italia baada ya kupuuzwa na kocha Thomas Tuchel ugani Stamford Bridge.

Katika mahojiano yake na Sky Sport Italia, Lukaku alifichua kwamba hafurahii maisha yake kambini mwa Chelsea.

“Sifurahii hali ilivyo hasa ikizingatiwa kwamba mimi ni mchapakazi. Hilo linanifanya kuwazia uwezekano wa kurejea Inter,” akasema Lukaku ambaye amefungia Chelsea mabao saba kutokana na mechi 18 tangu arejee kambini mwa mabingwa hao wa EPL 2016-17.

Lukaku alisajiliwa na Chelsea kwa mara ya kwanza mnamo 2011 akiwa na umri wa miaka 18 kutoka Anderlecht ya Ubelgiji. Ingawa hivyo, nyota yake haikung’aa ugani Stamford Bridge na akahamia kambini mwa West Brom kabla ya kujiunga baadaye na Everton kisha Manchester United kwa misimu miwili.

Aliingia katika sajili rasmi ya Inter mnamo Agosti 2019 na akafunga mabao 64 kutokana na mechi 95 huku akiongoza miamba hao kutwaa taji la Ligi Kuu ya Italia (Serie A) kwa mara ya kwanza baada ya miaka 11.

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

You can share this post!

Kiungo Mejbri wa Man-United ajumuishwa katika kikosi cha...

Pigo zaidi kwa Leicester baada ya Jamie Vardy pia kupata...

T L