• Nairobi
  • Last Updated May 9th, 2024 6:40 PM
Mabwanyenye wapya Newcastle nao pia wajishasha kuwania saini ya Mbappe

Mabwanyenye wapya Newcastle nao pia wajishasha kuwania saini ya Mbappe

Na MASHIRIKA

HUKU kandarasi yake akiwa PSG ya Ufaransa ikitarajiwa kukamilika mwishoni mwa msimu huu, kumeibuka tetesi kuwa nyota Kylian Mbappe (pichani) anawindwa kisawasawa na Newcastle United nchini Uingereza.

Newcastle chini ya umiliki mpya wa mabwenyenye waarabu kutoka Saudia, wanatarajiwa kuvunja benki ili kusajili nyota kadhaa mwishoni mwa msimu huu.Sasa wanalenga kumvutia straika huyo mahiri kwa kumpendekezea donge nono.Mbappe amekuwa akitaka kuondoka PSG huku vigogo wa Uhispania, Real Madrid, wakiwa mstari wa mbele kutwaa huduma zake.

Alikerwa kabla ya kuanza kwa msimu huu PSG ilipokataa kumuachilia aelekee Real, licha ya Rais Florentina Perez kuwa tayari kutoa kitita kikubwa.Kocha mpya Newcastle, Eddie Howe, anataka majina makubwa. Inaaminika analenga kuleta majina makubwa katika timu hiyo ili iweze kutoa ushindani mkubwa kwa timu ambazo zimetawala ligi ya Uingereza kama Manchester City, Manchester United, Liverpool, Chelsea, Arsenal na nyingine.

Uvumi kuwa huenda Mbappe akatua Newcastle umeshika kasi zaidi baada ya nyota wa zamani wa Arsenal na mwanadimba wa zamani wa Ufaransa Emmanuel Petit kuthibitisha kuna mpango.

You can share this post!

Mwendwa anaswa tena

Ajenti wa Bale achemkia mashabiki wa Real madrid kwa...

T L