• Nairobi
  • Last Updated May 11th, 2024 7:15 PM
Mamelodi Sundowns anayochezea Brian Mandela yapoteza rekodi ya kutoshindwa ligini

Mamelodi Sundowns anayochezea Brian Mandela yapoteza rekodi ya kutoshindwa ligini

Na GEOFFREY ANENE

BRIAN “Mandela” Onyango alitumiwa na Mamelodi Sundowns dakika 79 klabu hiyo yake ikipoteza rekodi ya kutoshindwa kwenye Ligi Kuu ya Afrika Kusini ya msimu huu kwa kuchapwa 2-1 na Kaizer Chiefs katika mechi yake ya 22, Jumapili.

Sundowns, ambayo ilikuwa nyumbani ugani Loftus Versfeld, ilitangulia kuona lango kupitia kwa mshambuliaji wa Uruguay, Gaston Sirino dakika ya 35.

“The Brazilians” jinsi Sundowns inafahamika kwa jina la utani, ilipoteza nafasi kadhaa nzuri na pia kuponea mashambulizi kadhaa hatari kabla ya beki Mosa Lebusa kujifunga alipogusa krosi ya mshambuliaji wa Serbia, Samir Nurkovic dakika ya 72.

Chiefs ilichukua uongozi 2-1 kupitia kwa kiungo Dumisani Zuma dakika mbili baadaye alipobaki pekee yake na kipa kabla ya Mandela kupumzishwa na nafasi yake kujazwa na raia wa Brazil Ricardo Nascimento.

Kabla ya kupigwa na Chiefs anayochezea kiungo Mkenya Anthony “Teddy” Akumu, Sundowns ilikuwa imezoa ushindi mara 13 na sare nane. Mabingwa watetezi Sundowns wamekalia juu ya jedwali la ligi hiyo ya klabu 16 kwa alama 47. Chiefs, ambayo haikutumia Akumu katik mchuano huo, inapatikana katika nafasi ya nane kwa alama 28 baada ya kujibwaga uwanjani mara 23.

You can share this post!

Ruto aiga Kibaki katika mpango wake wa kufufua uchumi...

Shikanda apigania taji la ligi na uwanja wa klabu