• Nairobi
  • Last Updated May 2nd, 2024 8:55 PM
Droo ya Klabu Bingwa Ulaya hatua ya 16-bora kufanywa upya muda mchache ujao baada ya kutokea kwa hitilafu za kiteknolojia leo mchana

Droo ya Klabu Bingwa Ulaya hatua ya 16-bora kufanywa upya muda mchache ujao baada ya kutokea kwa hitilafu za kiteknolojia leo mchana

Na MASHIRIKA

DROO ya Klabu Bingwa Ulaya hatua ya 16-bora kufanywa upya muda mchache ujao baada ya kutokea kwa hitilafu za kiteknolojia leo mchana.

Awali, kulitokea mpira wa Manchester United dhidi ya Villareal licha ya kwamba klabu hizo zilikutana katika awamu ya makundi.

Ingawa Man-U walikuwa wamepangiwa kukutana na Paris Saint-Germain (PSG) ya Ufaransa katika hatua ya 16-bora ya Klabu Bingwa Ulaya (UEFA) msimu huu wa 2021-22, sasa kila timu iliyofuzu hatua ya 16-bora itasubiri kujua wapinzani wapya.

Lingekuwa ni pambano la wachezaji wa haiba kubwa duniani – Lionel Messi wa PSG na Cristiano Ronaldo wa Man-United.

DROO YA HATUA YA 16-BORA YA UEFA 2021-22 ILIYOFUTILIWA MBALI:

Benfica vs Real Madrid

Villarreal vs Manchester City

Atletico Madrid vs Bayern Munich

Red Bull Salzburg vs Liverpool

Inter Milan vs Ajax

Sporting Lisbon vs Juventus

Chelsea vs Lille

PSG vs Manchester United

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

You can share this post!

Kidero, Orengo wahudhuria Azimio La Umoja badala ya korti

Rangers kumenyana na Dortmund kwenye mchujo wa Europa League

T L