Na MASHIRIKA
DROO ya Klabu Bingwa Ulaya hatua ya 16-bora kufanywa upya muda mchache ujao baada ya kutokea kwa hitilafu za kiteknolojia leo mchana.
Awali, kulitokea mpira wa Manchester United dhidi ya Villareal licha ya kwamba klabu hizo zilikutana katika awamu ya makundi.
Ingawa Man-U walikuwa wamepangiwa kukutana na Paris Saint-Germain (PSG) ya Ufaransa katika hatua ya 16-bora ya Klabu Bingwa Ulaya (UEFA) msimu huu wa 2021-22, sasa kila timu iliyofuzu hatua ya 16-bora itasubiri kujua wapinzani wapya.
Lingekuwa ni pambano la wachezaji wa haiba kubwa duniani – Lionel Messi wa PSG na Cristiano Ronaldo wa Man-United.
DROO YA HATUA YA 16-BORA YA UEFA 2021-22 ILIYOFUTILIWA MBALI:
Benfica vs Real Madrid
Villarreal vs Manchester City
Atletico Madrid vs Bayern Munich
Red Bull Salzburg vs Liverpool
Inter Milan vs Ajax
Sporting Lisbon vs Juventus
Chelsea vs Lille
PSG vs Manchester United
TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO