• Nairobi
  • Last Updated May 17th, 2024 2:31 PM
Man-Utd yamtega staa Antony na Sh7.2 bilioni

Man-Utd yamtega staa Antony na Sh7.2 bilioni

NA MASHIRIKA

MANCHESTER, UINGEREZA

‘MASHETANI WEKUNDU’ Manchester United wameweka mnadani Sh7.2 bilioni kumtwaa mshambulizi mahiri wa Ajax, Antony.

Hata hivyo, kiasi hicho kinaonekana bado kuwa chini na kile ambacho miamba hao wa Uholanzi wanataka.

Mbrazil Antony aling’ara kambini mwa Ajax msimu uliopita, akipachika wavuni mabao 12 na kumega pasi 10 zilizoishia kujaa nyavuni katika michuano 33 katika mashindano yote.

Alitia kimiani mabao manane na kufuma pasi nne ligini zilizochangia pakubwa klabu hiyo kubeba taji la ligi.

Kocha Erik ten Hag anaaminika kutamani sana kumvutia Antony ambaye amechezea Ajax mara 78 tangu awasili kutoka Sao Paulo mnamo Julai 2020. Antony amechangia jumla ya magoli 22 na pasi 20 zilizofungwa.

Tetesi nchini Uingereza zinaeleza kuwa mabingwa hao wa zamani wamesema wana Sh7.2 bilioni, ingawa Ajax wanataka Sh9.6 bilioni kwa sababu ya umuhimu wake kwenye klabu hiyo.

Ripoti zinasema kuwa maajenti wa Antony wanasukuma Ajax ikubali ada ya chini kwa sababu mchezaji mwenyewe ana hamu kubwa sana ya kuhamia uwanjani Old Trafford kabla ya soko kufungwa Septemba 1.

“Ni wazi kuwa tunataka kuendelea kuwa na Antony. Nadhani bado ana kandarasi nasi hadi 2025. Ningependa kufanya kazi naye na anajua hivyo na pia klabu inafahamu hayo,” kocha mpya wa Ajax, Alfred Schreuder alisema majuzi.

Antony amekuwa mkekani tangu Machi akiuguza jeraha la kifundo.

United imeratibiwa kuelekea nchini Thailand leo Ijumaa kwa mkondo wa kwanza wa maandalizi ya msimu mpya.

  • Tags

You can share this post!

Tutazungumza na Al-Shabaab kwa wakati mwafaka, asema Rais...

DRC, Rwanda zakubali kusitisha uadui wao

T L