• Nairobi
  • Last Updated May 18th, 2024 6:55 AM
Michuano ya ligi ya Mtwapa Primia yanoga Kilifi

Michuano ya ligi ya Mtwapa Primia yanoga Kilifi

NA CHARLES ONGADI

MICHUANO ya ligi ya Mtwapa Primia, Kilifi ilipamba moto katika uwanja wa shule ya msingi ya Mtwapa, Jumapili ambapo jumla ya mechi nne ziligaragazwa.

Custom Villa FC inayojivunia ufuasi mkubwa eneo la Mtwapa ilijipata kona mbaya ilipomizwa 2-0 na EPZ katika mtanange ambao Kenedy Maitha na Hamisi Mohammed walipachika mabao mawili ya haraka katika kipindi cha kwanza.

Starlight United FC nayo ikaiadhibu kinyama La Liga Youth kwa mabao 4-1. Ni mabao yaliyofungwa na Abdilahi Hassan, Anwar Bakari aliyepachika mawili kabla ya Emmanuel Ngari kudungilia msumari wa mwisho dakika ya 78. Bao la kufuitia machozi la La Liga lilifungwa a Francis Kimunyu katika muda wa ziada.

Nao La Liga Snr wakalipiza kwa kuinyuka Boda Boda 1-0 bao lililofungwa na Stephen Dio Chareli katika dakika ya 17.

Shule ya Upili ya Mtwapa nayo ikaifunza Blue Stars namna ya kusakata kabumbu kwa kuwacharaza 3-0 katika pambano la mwisho.

Michael Gereza alifungua ukurasa dakika ya 19 kisha Abubakar Mkoka akaongeza la pili dakika ya 34 kabla ya Geofrey Mwinga kufunga kazi dakika ya 76.

Michuano hii imeratibiwa kuchezwa kila siku ya Jumapili katika uwanja wa shule ya msingi ya Mtwapa kuanzia saa mbili asubuhi kwa lengo la kupalilia vipaji na wakati huo huo kuwaepusha vijana kujitumbukiza katika matumizi ya mihadarati.

You can share this post!

PAUKWA: Ulevi wamtosa mzee Yumbayumba majini

Wakazi wa mitaa sita ya Mukuru wahangaika kupata maji kwa...

T L