• Nairobi
  • Last Updated May 16th, 2024 8:50 PM
Muumini wa Kanisa la Kiadventista aponyoka na Sh11 milioni za bonasi ya Sportpesa Mega Jackpot

Muumini wa Kanisa la Kiadventista aponyoka na Sh11 milioni za bonasi ya Sportpesa Mega Jackpot

Na CECIL ODONGO

MWANAFAMASIA mwenye umri wa miaka 35 ameponyoka na Sh11 milioni za bonasi ya Sportpesa Mega Jackpot.

El Aden Wambita ambaye ni muumini wa Kanisa la Kiadventista, alituzwa pesa hizo jana katika Duka kubwa la Greenspan, mtaani Donholm.

Alikosa tu mechi kati ya Tottenham Hotspur dhidi ya Liverpool ambapo alikuwa amebashiri ingeishia sare ya 1-1 ila ikaishia 2-1 kwa manufaa ya Spurs.

Iwapo Joel Matip angekosa kujifunga dakika za mwisho, basi Wambita angeshinda Jackpot na kujizolea Sh326 milioni. Katika ubashiri huo alitumia tu Sh99 pekee.

Wambita ambaye alikiri kuwa yeye ni Mwadventista na anafuata kanuni za dini hiyo na aliandamana na mkewe Effie Wambita,, alisema kuwa kitu ambacho atafanya mwanzo ni kutoa fungu la kumi kwa kanisa.

“Nitatoa fungu la kumi kwa sababu naamini ni Mwenyezi Mungu ndiye aliniwezesha kushinda hela hizi. Nimefurahi sana na nilikuwa na uhakika kuwa ningepata bonasi hii baada ya kukosa pembamba Jackpot,” akasema Wambita.

Mshindi huyo anatoka Kaunti ya Homa Bay ila anafanya kazi hiyo ufamasia mjini Migori. Kwa kuwa anatoka familia ya watoto saba, analenga kutumia hela hizo kuwalipia wadogo wake karo na pia kuwasaidia wazazi wake.

Kuhusu debi ya Mashemeji ambayo itakuwa ikisakatwa Jumamosi hii, Wambita atakuwa akiomba Gor Mahia ishinde AFC Leopards. Katika ligi za Uingereza, Wambita anashabikia Manchester United.

  • Tags

You can share this post!

Demu aanika siri za ndoa yake, rafiki yake apindua ajenda...

Waziri wa Maji Alice Wahome aapa kushuka na wanaomchimba...

T L