NA JANET KAVUNGA
SHANZU, MOMBASA
MWANADADA wa hapa anajuta kuanika siri za ndoa yake kwa rafiki yake ambaye alizitumia kupindua serikali yake.
Demu alisema kwamba alikuwa akimwamini rafiki yake kiasi cha kumweleza aliyokuwa akipitia katika ndoa yake bila kujua mwenzake huyo alikuwa akimmezea mate mumewe.
Juzi, jamaa alimgombeza vikali na kumtimua akimlaumu kwa kutokomaa na kulinda siri za ndoa.
Demu alipompigia simu rafiki yake kumweleza yaliyomsibu, alimkejeli kwa kumtaka abebe msalaba wake mwenyewe kisha akazima simu.
Baada ya siku mbili alipata habari kwamba mumewe alikuwa ameoa aliyedhani alikuwa rafiki yake wa dhati.