• Nairobi
  • Last Updated May 2nd, 2024 5:50 AM
Demu aanika siri za ndoa yake, rafiki yake apindua ajenda kwa kukwachua mume

Demu aanika siri za ndoa yake, rafiki yake apindua ajenda kwa kukwachua mume

NA JANET KAVUNGA

SHANZU, MOMBASA

MWANADADA wa hapa anajuta kuanika siri za ndoa yake kwa rafiki yake ambaye alizitumia kupindua serikali yake.

Demu alisema kwamba alikuwa akimwamini rafiki yake kiasi cha kumweleza aliyokuwa akipitia katika ndoa yake bila kujua mwenzake huyo alikuwa akimmezea mate mumewe.

Juzi, jamaa alimgombeza vikali na kumtimua akimlaumu kwa kutokomaa na kulinda siri za ndoa.

Demu alipompigia simu rafiki yake kumweleza yaliyomsibu, alimkejeli kwa kumtaka abebe msalaba wake mwenyewe kisha akazima simu.

Baada ya siku mbili alipata habari kwamba mumewe alikuwa ameoa aliyedhani alikuwa rafiki yake wa dhati.

  • Tags

You can share this post!

Baba azuiliwa kwa madai ya kupiga na kuua bintiye...

Muumini wa Kanisa la Kiadventista aponyoka na Sh11 milioni...

T L