• Nairobi
  • Last Updated May 20th, 2024 9:16 PM
Mwanasoka wa zamani wa Harambee Stars, Ahmed Breik aaga dunia

Mwanasoka wa zamani wa Harambee Stars, Ahmed Breik aaga dunia

NA ABDULRAHMAN SHERIFF

MWANASOKA wa zamani wa kimataifa wa Kenya, Ahmed Breik alifariki Jumatatu Desemba 11, 2023 asubuhi nyumbani kwake eneo la Majengo Mvita, Mombasa, baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Akitoa habari za kifo hicho, mtoto wa tatu wa kiungo huyo wa zamani wa Feisal FC, Mombasa Combined na Harambee Stars, Ali Ahmed Breik amesema babake aliaga dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

“Hakuwa baba yetu pekee bali pia alikuwa ni rafiki yetu mkubwa. Kifo chake kimetuhuzunisha kwani tutakosa ushauri wake wa jinsi ya kufanikiwa maishani na mwongozo kama mzazi wetu,” amesema Ali ambaye yeye amewahi kuchezea Mombasa Stars, Mombasa Wanderers, Bandari na timu ya taifa ya Harambee Stars.

Swala ya mwisho ya marehemu Breik iliswaliwa katika Msikiti wa Marembo mara baada ya sala ya Alasiri (saa 10.00 jana jioni) na akazikwa kwenye makaburi ya Waislamu ya Kikowani.

Waombolezaji wakibeba mwili wa Ahmed Breik kuelekea makaburi ya Kikowani, Mombasa ambako alizikwa Desemba 11, 2023. Picha|Abdulrahman Sheriff

Mwanasoka mwenzake wa zamani wa timu ya Kenya, Nassir Omar amesema licha ya kuwa wapinzani katika ngazi ya klabu yeye akichezea Mwenge na marehgemu Feisal, walikuwa marafiki wakubwa na walicheza pamoja katika timu ya taifa.

“Nimesikitika kusikia kifo chake na natuma risala zangu za rambirambi kwa familia yake na kumuomba Mwenyezi Mungu amweke mahali pema penye wema,” amesema Omar katika risala yake ya kuomboleza kifo cha Breik.

Marehemu Breik aliwahi kuichezea timu ya taifa ya Kenya hadi mwaka 1975 lakjini aliendelea kuichezea klabu yake ya Feisal mpaka mwaka 1980 alipoacha kucheza.

Miaka ya nyuma aliwahi kuichezea timu ya East Africa Cargo Handling Services ambayo sasa ni Bandari FC.

Marehemu ameacha mjane, watoto saba wakiwemo wa kiume watatu na wa kike wanne na wajukuu watano.

  • Tags

You can share this post!

Azimio yaendelea kupasuka Wamalwa sasa akitofautiana na...

Siasa: Ukambani na Meru nao pia wasuka muungano mpya

T L