• Nairobi
  • Last Updated May 10th, 2024 1:50 PM
Nakuru West Queens washinda Eldoret Falcons 3-2 ugenini

Nakuru West Queens washinda Eldoret Falcons 3-2 ugenini

NA RICHARD MAOSI

TIMU ya Nakuru West Queens FC ambayo inashiriki Ligi ya Akinadada ya KWPL, inaenelea kufanya vyema ligini baada ya kushinda Eldoret Falcons 3-2 ugenini.

Diana Kosgei alisaidia timu ya Nakuru kutia wavuni magoli mawili huku Linda Kihara akifunga la tatu na la ushindi katika uwanja wa Eldoret Showground.

Nakuru walipata goli la kwanza kunako dakika ya 15, kupitia juhudi za mchezaji Diana Koskei ambaye aliacha madifenda wakiwa hoi .

Linda Kihara alipatia timu yake goli la pili kunako dakika ya 53 kabla ya wapinzani wao Eldoret Falcons kurejesha bao dakika tano baadae.

Kipindi cha pili timu zote zilionyesha soka ya hali ya juu, huku wakiendelea kushambuliana kwa zamu hadi dakika ya 77 Diana alipoongezea Nakuru Queens goli la pili.

Linda Nasimiyu aliongezea timu yake bao la tatu kunako dakika ya 83 na kuhakikishia timu yake ushindi huo muhimu, ambao umeweka Nakuru Queens pazuri ligini.

Nakuru Queens wamepanda nafasi mbili ligini, huku Eldoret Falcons wakiendelea kuvuta mkia.

Katika mechi ijayo Nakuru West Queen watakabiliana na Trans-Nzoia Falcons, mchuano ambao utachezwa kwenye uwanja wa Nakuru Showground tarehe 20 Machi 2021.

Huku Oserian Ladies wakipambana na Vihiga Queens siku ya Jumapili katika kaunti ndogo ya Naivasha.

Mkufunzi wa Nakuru West Queens Peterson Esitoko anatarajia kuwa, wachezaji wake wataendeleza wimbi la matokea mazuri.

Nakuru wamejizatiti kuendeleza mazoezi katika uwanja wa Shabbab Grounds.

Wachezaji wa Nauru West Queens wakifanya mazoezi uwanjani Shabbab Nakuru.

You can share this post!

Binti wa chuo aeleza anavyovuna Sh300,000 kila mwezi...

Makinda wa Nakuru walenga kuchezea Harambee Stars